Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kujifunza

Kujifunza

Kwa nini ni lazima Mkristo ajifunze Neno la Mungu kwa ukawaida?

Zb 1:​1-3; Met 18:15; 1Ti 4:6; 2Ti 2:15

Tazama pia Mdo 17:11

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Da 9:​1-3, maelezo ya chini—Baada ya kujifunza vitabu vitakatifu, nabii Danieli anatambua kwamba ile miaka 70 ya kukaa uhamishoni imekaribia kwisha

    • Zb 119:​97-101—Mtunga zaburi aliyeongozwa na roho anaeleza jinsi anavyoipenda sheria ya Mungu na kutaja manufaa anayopata kwa kuitumia maishani mwake

Kwa nini tunahitaji kuendelea kupata ujuzi?

Ebr 6:​1-3; 2Pe 3:18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Met 4:18—Kama tu nuru ya asubuhi inavyong’aa zaidi na zaidi, ndivyo Yehova anavyoendelea kufanya kweli iwe wazi zaidi kwa watu wanaompenda Mungu

    • Mt 24:​45-47—Yesu anatabiri kwamba atamweka rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ambaye atakuwa na jukumu la kuandaa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa katika siku za mwisho

Kwa nini tunapaswa kuthamini zaidi hekima ya Biblia kuliko hekima yoyote inayopatikana katika vitabu vya falsafa za wanadamu?

Yehova anaahidi kuwapatia nini wale ambao wanajifunza Biblia kwa unyoofu?

Tunahitaji kumwomba nini Yehova katika sala ili tunufaike kutokana na funzo letu la kibinafsi la Biblia?

Kwa nini tunapaswa kutumia kikamili maandalizi yote ya chakula cha kiroho kutoka kwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”?

Kwa nini tunapaswa kutafuta ujuzi sahihi, na kukazia uangalifu hata mambo madogo-madogo?

Kwa nini ni muhimu sana kwetu kupata hekima na uelewaji?

Kwa nini tunapaswa kusoma kwa mwendo wa polepole na kutafakari kuhusu mambo tunayosoma?

Kwa nini tunapaswa kufikiria kuhusu jinsi tunavyoweza kulitumia Neno la Mungu maishani mwetu?

Kwa nini tunapaswa kutafakari kuhusu jinsi tunavyoweza kushiriki na wengine mambo ambayo tumejifunza?

Tunaweza kunufaikaje ikiwa tutajifunza tena na tena kweli muhimu?

2Pe 1:13; 3:​1, 2

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Kum 6:​6, 7; 11:​18-20—Yehova anawaagiza watu wake wayakazie maneno yake kwa watoto wao, wawafundishe maneno yake kwa kuyarudia-rudia

Tunapata manufaa gani tunapozungumzia Neno la Mungu tukiwa familia?

Efe 6:4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 18:​17-19—Yehova anataka Abrahamu awafundishe watu wa nyumba yake ili waifuate njia ya uadilifu

    • Zb 78:​5-7—Katika Israeli, kila kizazi kilipaswa kuwafundisha watoto wao kumhusu Yehova ili kizazi kinachofuata kiendelee kumtumaini Yehova

Kujifunza pamoja na kutaniko kunatusaidiaje?

Ebr 10:25

Tazama pia Met 18:1