Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hekima

Hekima

Tunahitaji kuwa na mtazamo gani ili tupate hekima ya kweli?

Tunaweza kupata wapi hekima ya kweli?

Je, ni jambo linalofaa kumwomba Mungu atupatie hekima?

Kol 1:9; Yak 1:5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Nya 1:​8-12—Mfalme kijana Sulemani anasali ili apate hekima itakayomsaidia kutawala Israeli kwa njia inayofaa, na Yehova anafurahi kumpatia jambo aliloomba

    • Met 2:​1-5—Hekima, uelewaji, na utambuzi zinahusianishwa na hazina zilizofichika ambazo tunanufaika tunapozitafuta, na Yehova huwathawabisha wale wanaozitafuta sifa hizo kwa bidii

Yehova anatupatia hekima kupitia nani na kwa msaada wa nini?

Isa 11:2; 1Ko 1:​24, 30; 2:13; Efe 1:17; Kol 2:​2, 3

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Met 8:​1-3, 22-31—Hekima ya Mungu inafafanuliwa kuwa mtu, na ufafanuzi huo unamfaa Yesu ambaye aliumbwa na Yehova kabla ya vitu vingine vyote

    • Mt 13:​51-54—Watu wengi wanaomsikiliza Yesu hawaelewi jinsi mwanamume ambaye amelelewa miongoni mwao anaweza kuwa na hekima nyingi hivyo

Ni sifa gani zinazoonyesha kwamba tuna hekima ya Mungu?

Hekima inatupatia mwongozo na ulinzi gani maishani?

Hekima ya Mungu ina thamani nyingi kadiri gani?

Met 3:​13, 14; 8:11

Tazama pia Ayu 28:18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ayu 28:​12, 15-19—Ingawa anateseka sana kwa sababu ya huzuni, maumivu, na kupoteza mali zake, Ayubu anaeleza jinsi anavyothamini sana hekima ya Mungu

    • Zb 19:​7-9—Mfalme Daudi anasema kwamba sheria na vikumbusho vya Yehova vinaweza kuwapatia hekima hata wale wasio na uzoefu

Hekima ya ulimwengu, inayompuuza Mungu, inaweza kutudhuru kwa njia gani?