Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kazi

Kazi

Kuna uhusiano gani kati ya kazi na shangwe?

Ni zipi baadhi ya faida za kufanya kazi vizuri na kwa ustadi?

Met 22:29

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 16:​16-23—Kijana Daudi anajipatia sifa kwa kuwa mwanamuziki mwenye ustadi, ujuzi unaomwezesha kumsaidia mfalme wa Israeli mwenye matatizo

    • 2Nya 2:​13, 14—Kwa sababu ya ustadi wake akiwa fundi, Hiram-abi anatumiwa na Mfalme Sulemani katika kazi kubwa ya ujenzi

Watumishi wa Yehova wanataka kujulikana kuwa wafanyakazi wa aina gani?

Efe 4:28; Kol 3:23

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 24:​10-21—Rebeka anafanya mengi zaidi ya mambo anayoombwa kufanya na mtumishi wa Abrahamu, hivyo anaonyesha roho ya kuwasaidia wengine na bidii

    • Flp 2:​19-23—Mtume Paulo anamkabidhi mwanamume kijana Timotheo mgawo mzito kwa sababu ya utayari wake wa kufanya kazi kwa bidii na unyenyekevu

Kwa nini watumishi wa Mungu wanajitahidi kuepuka mwelekeo wowote wa kuwa wavivu?

Met 13:4; 18:9; 21:​25, 26; Mhu 10:18

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Met 6:​6-11—Mfalme Sulemani anamtumia chungu kufundisha masomo kuhusu kufanya kazi kwa bidii na kuepuka uvivu

Kwa nini tunapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kushughulikia mahitaji yetu?

Kwa nini tunapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuwatunza watu wa familia wanaotutegemea?

1Ti 5:8

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

Wakristo wanapaswa kuwa tayari kutumiaje mapato wanayopata kutokana na kazi yao ngumu?

Tunapaswa kuwa na mtazamo gani wenye usawaziko kuelekea mshahara tunaopata tunapofanya kazi ya kimwili?

Tunajuaje kwamba Yehova anataka kutusaidia tufanye kazi yetu vizuri na kushughulikia mahitaji yetu ya kimwili?

Mt 6:​25, 30-32; Lu 11:​2, 3; 2Ko 9:10

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 31:​3-13—Labani anamtendea isivyo haki Yakobo, mkwe wake na mfanyakazi wake, lakini Yehova anamwona Yakobo akifanya kazi kwa bidii, naye anambariki

    • Mwa 39:​1-6, 20-23—Yehova anabariki kazi ya Yosefu, akiwa mtumwa kwenye nyumba ya Potifa na akiwa mfungwa gerezani

Kwa nini kazi yetu ya kimwili haipaswi kamwe kuwa muhimu zaidi kuliko utumishi wetu kwa Mungu?

Zb 39:​5-7; Mt 6:33; Yoh 6:27

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 12:​15-21—Yesu anatoa mfano unaoonyesha kwamba ni upumbavu kufikiri kwamba kufanya kazi ili kupata pesa ni muhimu zaidi ya kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu

    • 1Ti 6:​17-19—Mtume Paulo anawaonya Wakristo matajiri kuhusu hatari ya kuwa na majivuno na anawatia moyo wawe “matajiri katika matendo mazuri”

Tunapaswa kuongozwa na kanuni gani tunapochagua kazi?

Kufanya kazi kwa ajili ya Yehova

Kazi iliyo muhimu zaidi kwa Wakristo ni ipi?

Kwa nini tuna hamu ya kujitahidi kufanya yote tuwezayo katika utumishi wa Yehova?

Kwa nini hatupaswi kutarajia kwamba watumishi wote wa Yehova wanaweza kutimiza mambo yaleyale katika utumishi Wake?

Gal 6:​3-5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mt 25:​14, 15—Mfano wa Yesu unaonyesha kwamba hatarajii wafuasi wake wote watimize kiwango kilekile cha kazi

    • Lu 21:​2-4—Kwa fadhili, Yesu anatambua thamani kubwa ya mchango mdogo sana unaotolewa na mjane maskini

Tunatoa wapi nguvu za kutimiza kazi ambayo tumepewa tufanye katika utumishi wa Yehova?

2Ko 4:7; Efe 3:​20, 21; Flp 4:13

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • 2Ti 4:17—Mtume Paulo anakiri kwamba alipokea nguvu alizohitaji wakati alipozihitaji

Kwa nini tunapata shangwe tunapofanya kazi kwa bidii katika utumishi wa Yehova?