Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kazi

Kazi

Kuko upatano gani kati ya kazi na furaha?

Kujifunza kufanya kazi muzuri na kwa ufundi iko na faida gani?

Mez 22:29

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 16:​16-23—Kijana Daudi anajulikana kuwa mupiga-muziki mwenye ufundi, na anapata nafasi ya kumutumikia mufalme Sauli mwenye anavurugika mu akili

    • 2Ny 2:​13, 14—Juu iko na ufundi wa kutengeneza vitu mbalimbali, Hiram-abi anatumika na Mufalme Sulemani mu kazi kubwa ya ujenzi

Watumishi wa Yehova wanapenda kujulikana kuwa wafanyakazi wa namna gani?

Efe 4:28; Kol 3:23

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 24:​10-21—Rebeka anafanyia mutumishi wa Abrahamu mengi zaidi ya ile yenye alimuomba; na ile inaonyesha kama iko na roho ya kusaidia wengine na iko na bidii

    • Flp 2:​19-23—Mutume Paulo anapatia kijana Timoteo daraka nzito juu iko tayari kutumikia wengine kwa bidii na kwa unyenyekevu

Juu ya nini watumishi wa Mungu wanajikazaka sana kuepuka uvivu?

Mez 13:4; 18:9; 21:​25, 26; Muh 10:18

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Mez 6:​6-11—Mufalme Sulemani anatumia mufano wa siafu juu ya kufundisha watu ulazima wa kutumika kwa bidii na kuepuka uvivu

Juu ya nini tunapaswa kutumika sana juu ya kutimiza mahitaji yetu?

Juu ya nini tunapaswa kutumika sana juu ya kusaidia watu wa familia wenye wako na lazima ya musaada wetu?

1Ti 5:8

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

Wakristo wanapaswa kufanya nini na vitu vyenye wanapata mu kazi yao?

Ni mawazo gani yenye usawaziko yenye tunapaswa kuwa nayo juu ya mushahara wenye tunapata mu kazi yetu?

Tunajua namna gani kama Yehova anapendaka kutusaidia tutumike muzuri na tutimize mahitaji yetu ya kimwili?

Mt 6:​25, 30-32; Lu 11:​2, 3; 2Ko 9:10

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 31:​3-13—Labani anamutendea Yakobo, bwana ya mutoto wake na pia mufanyakazi wake, bila haki, lakini Yehova anaona bidii ya Yakobo na anamubariki

    • Mwa 39:​1-6, 20-23—Yehova anabariki kazi ya Yosefu wakati iko mutumwa wa Potifa na wakati iko mu gereza

Juu ya nini kazi yetu ya kimwili haipaswe kuwa ya maana sana kuliko utumishi wetu kwa Mungu?

Zb 39:​5-7; Mt 6:33; Yoh 6:27

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Lu 12:​15-21—Yesu anatoa mufano juu ya kuonyesha kama ni upumbavu kutia vitu vya kimwili pa nafasi ya kwanza kuliko mambo ya kiroho

    • 1Ti 6:​17-19—Mutume Paulo anaonya Wakristo matajiri juu ya hatari ya kuwa wenye majivuno, na anawatia moyo wakuwe “matajiri katika matendo ya muzuri”

Ni kanuni gani zenye zinapaswa kutuongoza wakati tunapenda kukamata maamuzi kuhusu kazi?

Kazi ya Yehova

Ni kazi gani ya maana sana yenye Wakristo wanapaswa kufanya?

Juu ya nini tunapenda sana kufanya yetu yote mu kazi ya Yehova?

Juu ya nini hatupaswe kutazamia kama watu wote watamutumikia Yehova mu njia ileile?

Gal 6:​3-5

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mt 25:​14, 15—Mufano wa Yesu unaonyesha kama hatazamie wafuasi wake wamutumikie kwa kiasi ileile

    • Lu 21:​2-4—Yesu anaonyesha kama muchango kidogo sana wenye mujane maskini anatoa ni wa maana sana

Ni nani anatupatiaka nguvu ya kutimiza kazi yenye tunapewa mu utumishi wetu kwa Yehova?

2Ko 4:7; Efe 3:​20, 21; Flp 4:13

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • 2Ti 4:17—Mutume Paulo anaonyesha kama kwa wakati yenye kufaa alipata nguvu yenye alikuwa nayo lazima

Juu ya nini kutumika kwa bidii mu kazi ya Yehova kunaletaka furaha?