Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ibada

Ibada

Ni nani tu njo tunapaswa kuabudu?

Kut 34:14; Kum 5:​8-10; Isa 42:8

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mt 4:​8-10—Shetani anaambia Yesu kama ikiwa anamuabudu, atamupatia falme zote za dunia; Yesu anakatala kufanya vile, anaazimia kumuabudu tu Yehova

    • Ufu 19:​9, 10—Malaika mwenye nguvu anakatala mutume Yohana amuabudu

Yehova anatazamia tumuabudu namna gani?

Yoh 4:24; Yak 1:​26, 27

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Isa 1:​10-17—Yehova hapendi watu wenye hawaishi kulingana na kanuni zake wamuabudu kwa unafiki

    • Mt 15:​1-11—Yesu anaonyesha kama Yehova hapendake watu wamuabudu juu tu ya kumuabudu, ni kusema kutia kanuni za wanadamu pa nafasi ya kwanza kuliko sheria za Mungu

Kadiri inawezekana, tunapaswa kumuabudu Yehova pamoya na nani?

Ebr 10:​24, 25

Ona pia Zb 133:​1-3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 2:​40-42—Mu karne ya kwanza, Wakristo walikuwa nakutana juu ya kusali, kupitisha wakati pamoya, na kujifunza maandiko matakatifu

    • 1Ko 14:​26-40—Mutume Paulo anaagiza kama mikutano inapaswa kufanyika kwa utaratibu na inapaswa kuwa yenye kutia moyo juu kila mutu ajifunze na aelewe mambo yenye inafundishwa kule

Tunapaswa kufanya nini juu ya kuhakikisha kama Yehova anakubali ibada yetu?

Mt 7:​21-24; 1Yo 2:17; 5:3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Ebr 11:6—Mutume Paulo anafasiria kama imani ni ya lazima sana ikiwa tunapenda kumuabudu Yehova mu njia yenye anakubali

    • Yak 2:​14-17, 24-26—Yakobo, ndugu ya Yesu, anafasiria kama imani yetu inapaswa kusindikizwa na matendo na kama inapaswa kutuchochea kutenda