Mambo ya kufanya juu upate faida wakati uko najifunza hii broshua
Uombe mutu akufundishe: Uombe mutu mwenye alikupatia hii broshua akuwe anajifunza na weye Biblia, ao ufungule site yetu jw.org na uombe mutu wa kujifunza naye.
SEHEMU YA KWANZA
Soma kila fungu, ulizo yenye kuwa juu ya kila fungu (A) na maandiko (B) yenye inakazia mawazo makubwa. Utaona pia kama maandiko fulani iko na neno “soma.”
SEHEMU YA KATIKATI
Maneno ya kwanza-kwanza (C) yenye iko chini ya sehemu Tujifunze Mambo Mingi Zaidi inaonyesha mambo yenye itazungumuziwa. Vichwa vidogo-vidogo (D) vinaonyesha mawazo makubwa yenye itazungumuziwa. Soma maandiko, tafuta majibu ya maulizo, na uangalie video (E).
Angalia picha na usome maelezo yenye iko karibu na picha (F), na ufikirie namna unaweza kujibia ulizo ao maulizo yenye iko mu sehemu Watu Fulani Wanasemaka (G).
SEHEMU YA MWISHO
Kwa Kifupi na Maulizo ya kujikumbusha (H) njo sehemu zenye zinamalizia somo. Andika tarehe yenye mumemaliza kujifunza somo fulani. Sehemu Pima kufanya hivi (I) inakuonyesha jambo ya kufanya juu ujifunze mambo mingi zaidi ao juu utumikishe mambo yenye umejifunza. Mu sehemu Habari Zingine (J) muko mambo ingine yenye, kama unapenda, unaweza kusoma ao kuangalia.
Namna ya kutafuta maandiko mu Biblia
Andiko inaonyeshwa na jina ya kitabu ya Biblia (A), sura (B), na mustari ao mistari (C). Kwa mufano, Yohana 17:3 maana yake kitabu ya Yohana, sura ya 17, mustari wa 3.