Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua ya Baraza Yenye Kuongoza

Barua ya Baraza Yenye Kuongoza

Ndugu na Dada Wapendwa:

Kumupenda Mungu na kupenda watu njo inatuchocheaka ‘tuende. . . na tufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na tuwabatize.’ (Mt. 28:19, 20; Mk. 12:28-31) Upendo wa kweli unakuwaka na nguvu. Unaweza kugusa mioyo ya wale wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele.”​—Mdo. 13:48.

Zamani, tulikuwaka nahangaikia kuweka mu akili namna ya kuanzisha mazungumuzo na kutolea watu vichapo. Lakini sasa, tunapenda kukomalisha sifa zenye zinaweza kutusaidia tuzungumuze muzuri zaidi na watu. Tunapenda kuonyesha watu upendo kwa kuzungumuzia habari zenye wao wanafurahia. Juu ya kufanya vile, tunapaswa kujipatanisha na hali ya mutu na kujua mambo yenye inamufurahishaka na yenye iko namuhangaisha. Namna gani hii broshua itatusaidia kufanya vile?

Hii broshua iko na somo 12. Kila somo inazungumuzia sifa yenye tunapaswa kutumikisha juu ya kuonyesha mutu upendo na kumufanya kuwa mwanafunzi. Mu kila somo muko habari fulani ya Biblia, yenye inazungumuzia namna Yesu ao mweneza-injili fulani wa mu karne ya kwanza alionyesha sifa fulani mu mahubiri. Kusudi ya hii broshua haiko tu kuweka mu akili namna fulani ya kuanzisha mazungumuzo, lakini ni kutafuta namna mbalimbali za kuonyesha watu upendo. Ni kweli kama tunapaswa kutumikisha kila sifa mu aina zote za mahubiri. Lakini, tutazungumuzia namna sifa fulani zinaweza kusaidia, zaidi sana wakati tunatembelea mutu kwa mara ya kwanza, wakati tunarudilia mutu, ao wakati tunaongoza funzo ya Biblia.

Wakati uko najifunza somo fulani, ufikiri sana juu ya namna unaweza kutumikisha sifa yenye kuzungumuziwa mu ile somo wakati uko nazungumuza na watu. Ujikaze umupende sana Yehova na watu. Zaidi ya kuwa tu na ufundi fulani, ile upendo njo itakusaidia ufanye wanafunzi.

Tunafurahia sana pendeleo kubwa ya kutumika bega kwa bega pamoya na nyiye. (Sef. 3:9) Yehova awabariki sana vile munaendelea kupenda watu na kufanya wanafunzi!

Ndugu zenu,

Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova