Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 1

Kupendezwa na Watu

Kupendezwa na Watu

Kanuni: “Upendo . . . hautafute faida zake wenyewe.”​—1 Ko. 13:4, 5.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Yohana 4:6-9. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Yesu alitambua nini juu ya ule mwanamuke mbele ya kuanza kuzungumuza naye?

  2.   Yesu alisema: “Nipatie maji nikunywe.” Juu ya nini ile ilikuwa njia ya muzuri ya kuanzisha mazungumuzo?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Mazungumzo yetu itakuwa ya muzuri kama tunaanza na habari yenye inafurahisha musikilizaji.

Umuige Yesu

3. Ujipatanishe na hali. Usianze mazungumzo vile tu weye ulipanga mu akili. Uanze na habari ya sasa yenye wengine wako wanafikiria. Ujiulize hivi:

  1.    ‘Kuko habari gani za sasa?’

  2.   ‘Ni habari gani njo majirani wangu, wafanyakazi wenzangu, na wanafunzi wenzangu wako nazungumuzia?’

4. Ukuwe muangalifu. Ujiulize hivi:

  1.    ‘Huyu mutu iko nafanya nini? Pengine iko nawaza nini?’

  2.   ‘Namna alishavala, namna anaonekana, na pia nyumba yake vinaonyesha nini juu ya imani yake na desturi yake?’

  3.   ‘Itakuwa muzuri kama naongea naye hii saa?’

5. Usikilize.

  1.    Usiseme mambo mingi.

  2.   Umusaidie mwenye uko naongea naye ajisikie huru kusema mawazo yake. Kama ni muzuri umuulize maulizo.