KUANZISHA MAZUNGUMZO

SOMO LA 1

Kupendezwa na Watu

Kupendezwa na Watu

Kanuni: “Upendo . . . hautafuti faida zake wenyewe.”—1 Kor. 13:​4, 5.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 4:​6-9. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Yesu aliona nini kabla ya kuanzisha mazungumzo?

  2.   Yesu akamwambia: “Naomba maji ninywe.” Kwa nini hiyo ilikuwa njia bora ya kuanzisha mazungumzo?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunaweza kuwa na mazungumzo mazuri ikiwa tutaanza kuzungumzia habari inayompendeza mtu.

Mwige Yesu

3. Badilika kulingana na hali. Usilazimishe kuanzisha mazungumzo kutokana na habari uliyopanga kuzungumzia. Anzisha mazungumzo kuhusu mambo ambayo watu wanafikiria siku hiyo. Jiulize:

  1.    ‘Taarifa za habari zinazungumzia nini?’

  2.   ‘Majirani, wafanyakazi, au wanafunzi wenzangu wanazungumzia mambo gani?’

4. Uwe mwenye utambuzi. Jiulize:

  1.    ‘Mtu huyu anafanya nini sasa? Huenda anafikiria mambo gani?’

  2.   ‘Mavazi, mwonekano, au nyumba yake inaonyesha nini kuhusu mambo anayoamini au utamaduni wake?’

  3.   ‘Je, huu ni wakati unaofaa kuzungumza naye?’

5. Sikiliza.

  1.    Usizungumze kupita kiasi.

  2.   Mtie moyo ashiriki mazungumzo. Ikiwa inafaa, muulize maswali.