Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

KUANZISHA MAZUNGUMZO

SOMO LA 2

Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida

Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida

Kanuni: “Neno linalosemwa wakati unaofaa —ni jema sana!”—Met. 15:23.

Filipo Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Matendo 8:​30, 31. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Filipo alianzishaje mazungumzo?

  2.   Kwa nini hiyo ilikuwa njia ya kawaida ya kuanzisha mazungumzo na kumfundisha mwanamume huyo jambo jipya?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Filipo?

2. Ikiwa tutazungumza kwa njia ya kawaida, huenda mtu huyo akahisi vizuri zaidi na akawa tayari kusikiliza ujumbe wetu.

Mwige Filipo

3. Uwe mwenye utambuzi. Unaweza kujua mambo mengi kumhusu mtu kwa kutazama ishara za uso na mwili wake. Je, mtu huyo anaonekana yuko tayari kuzungumza nawe? Unaweza kuanzisha mazungumzo kuhusu kweli ya Biblia kwa kusema, “Je, ulijua kwamba . . . ?” Usimlazimishe mtu ambaye hataki kuzungumza nawe.

4. Uwe na subira. Usihisi kwamba ni lazima uanze mara moja kwa kuzungumzia kweli ya Biblia. Subiri wakati unaofaa ili uzungumzie kweli hiyo kwa njia ya kawaida. Huenda hilo likamaanisha kusubiri mpaka wakati mwingine utakapozungumza tena na mtu huyo.

5. Badilika kulingana na hali. Huenda mtu akazungumza jambo ambalo hukutarajia. Hivyo, uwe tayari kuzungumzia habari itakayomfaa mtu huyo, hata ikiwa mtazungumzia kweli ya Biblia tofauti na ile uliyopanga.