Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 3

Fazili

Fazili

Kanuni: “Upendo ni . . . wenye fazili.”​—1 Ko. 13:4.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Yohana 9:1-7. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Nini njo Yesu alifanya kwanza; kuponyesha ule mwanaume kipofu ao kumuhubiria habari njema?​—Ona Yohana 9:35-38.

  2.   Unawaza ile ilifanya ule mutu afurahie kusikiliza habari njema?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Mutu anaweza kufurahia kusikiliza ujumbe wetu kama anaona kuwa tunamuhangaikia.

Umuige Yesu

3. Ujitie pa nafasi ya mutu. Pima kufikiria namna iko najisikia.

  1.    Ujiulize hivi: Pengine nini njo iko nahangaisha huyu mutu? Pengine nini njo inaweza kumusaidia na kumufurahisha? Kujiuliza ile maulizo kunaweza kukusaidia umuonyeshe fazili kutoka ku moyo na bila kulazimishwa.

  2.   Onyesha kama unahangaikia mambo yenye ule mutu anaona kuwa ya maana kwa kumusikiliza. Kama anakuambia namna iko najisikia ao mambo yenye iko namuhangaisha, usimukatize.

4. Zungumuza kwa fazili na kwa heshima. Namna unaongea na mutu inaweza kuonyesha kama unamuhangaikia na kama unataka kumusaidia. Chagua muzuri maneno yenye utasema na namna utaisema, na uepuke kusema maneno yenye itamufanya ajisikie mubaya.

5. Ukuwe tayari kusaidia. Tafuta nafasi za kusaidia mutu kwa kumupatia kitu fulani ao kumufanyia jambo fulani. Matendo ya fazili inaweza kukufungulia njia ya kuanzisha mazungumzo.