KUANZISHA MAZUNGUMZO

SOMO LA 3

Fadhili

Fadhili

Kanuni: “Upendo ni wenye . . . fadhili.”—1 Kor. 13:4.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 9:​1-7. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Yesu alifanya nini kwanza—alimponya mwanamume kipofu au alimhubiria habari njema?—Ona Yohana 9:​35-38.

  2.   Unafikiri kwa nini mwanamume huyo alikuwa tayari kumsikiliza Yesu alipomhubiria habari njema?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Huenda mtu akawa tayari kusikiliza ujumbe wetu ikiwa atahisi kwamba tunamjali.

Mwige Yesu

3. Uwe mwenye huruma. Jaribu kuwazia jinsi mtu huyo anavyohisi.

  1.    Jiulize: ‘Anahangaishwa na mambo gani? Ni mambo gani yanayoweza kumsaidia na kumvutia?’ Kufanya hivyo kutakusaidia uonyeshe fadhili kwa njia ya kawaida na ya unyofu.

  2.   Onyesha kwamba unajali mambo yanayomhangaisha mtu kwa kumsikiliza. Akikueleza jinsi anavyohisi kuhusu jambo fulani au tatizo analokabili, usibadili mazungumzo.

4. Zungumza kwa fadhili na heshima. Jinsi unavyozungumza itaonyesha unamhurumia mtu huyo na kwa kweli unataka kumsaidia. Uwe mwangalifu kuhusu kile unachosema na jinsi unavyosema, epuka kusema mambo yanayoweza kumkasirisha.

5. Toa msaada. Tafuta nafasi zinazofaa za kumsaidia mtu huyo kwa njia hususa. Tunapomwonyesha mtu fadhili, itakuwa rahisi kuanzisha mazungumzo.