Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 4

Unyenyekevu

Unyenyekevu

Kanuni: “Kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi.”​—Flp. 2:3.

Mambo Yenye Paulo Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 26:2, 3. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Namna gani Paulo alionyesha unyenyekevu wakati alikuwa nazungumuza na Mufalme Agripa?

  2.   Namna gani Paulo alimusaidia afikirie zaidi Yehova na Maandiko kuliko kumufikiria yeye?​—Ona Matendo 26:22.

Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?

2. Wakati tunazungumuza na watu kwa unyenyekevu na heshima, watafurahia zaidi ujumbe wetu.

Umuige Paulo

3. Uepuke kujionyesha. Wakati uko nazungumuza na mutu, usifanye ionekane sawa vile weye njo unajua kila kitu na kama ule mwenye uko naongea naye hajue kitu. Zungumuza naye kwa heshima.

4. Onyesha kabisa kama kweli zenye uko nafundisha zinatoka njo mu Biblia. Mu Neno ya Mungu muko mawazo yenye inaweza kugusa mioyo ya watu. Wakati tunaitumikisha, tutawasaidia wakuwe na imani ya kweli yenye inategemea Neno ya Mungu.

5. Ukuwe mupole. Usikaze mutu aitike mambo yenye unasema. Hatupende kubishana. Onyesha unyenyekevu kwa kubakia kimya ao kuondoka kama inafaa. (Mez. 17:14; Tit. 3:2) Tendo ya upole inaweza kufanya ule mutu akubali kuzungumuza na siye hata wakati ingine.