Paulo alionyeshaje unyenyekevu kwa jinsi alivyozungumza na Mfalme Agripa?
Paulo alimkaziaje fikira Yehova na Maandiko? —Ona Matendo 26:22.
Tunajifunza Nini Kutoka kwa Paulo?
2. Tukizungumza kwa unyenyekevu na heshima, ujumbe wetu utavutia zaidi.
Mwige Paulo
3. Zungumza kwa heshima. Epuka mtazamo wa kujionyesha kwamba unajua kila kitu na mtu unayezungumza naye hajui chochote.
4. Onyesha wazi kwamba msingi wa kweli unazofundisha ni Biblia. Neno la Mungu lina mawazo yanayogusa mioyo ya watu. Tunapolitumia, tunajenga imani yao katika msingi unaofaa.
5. Endelea kuwa mpole. Usijaribu kuendelea kuthibitisha kwamba uko sahihi. Hatutaki kubishana na watu. Onyesha unyenyekevu kwa kuwa mtulivu na kutambua wakati wa kuondoka. (Met. 17:14; Tito 3:2) Ukizungumza kwa upole, huenda mtu huyo akasikiliza ujumbe wetu wakati ujao.