Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

KUANZISHA MAZUNGUMZO

SOMO LA 5

Busara

Busara

Kanuni: “Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote.”—Kol. 4:6.

Paulo Alifanya Nini

1. Tazama VIDEO, au soma Matendo 17:​22, 23. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Paulo alihisije kuhusu mazoea ya dini za uwongo aliyoona katika jiji la Athene?—Ona Matendo 17:16.

  2.   Badala ya kuwahukumu Waathene, Paulo alitumiaje kwa busara mambo waliyoamini kama njia ya kuwahubiria habari njema?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Paulo?

2. Huenda watu wakatusikiliza zaidi ikiwa tutachagua kwa uangalifu mambo tutakayozungumza, jinsi tutakavyozungumza na wakati wa kuzungumza.

Mwige Paulo

3. Chagua maneno yanayofaa. Kwa mfano, unapozungumza na mtu ambaye si Mkristo, huenda ukahitaji kubadili jinsi unavyoitaja Biblia au unavyomrejelea Yesu.

4. Usiwe na haraka ya kumkosoa mtu. Mruhusu ajieleze. Ikiwa atasema jambo lolote lisilopatana na mafundisho ya Biblia, usibishane naye. (Yak. 1:19) Ukimsikiliza, utajua mambo anayoamini na kwa nini anayaamini.—Met. 20:5.

5. Kubaliana naye na mpongeze inapofaa kufanya hivyo. Huenda anaamini kwamba mafundisho ya dini yake ni sahihi. Kwanza, jaribu kuzungumzia mambo mnayokubaliana, kisha msaidie hatua kwa hatua aelewe mambo ambayo Biblia inafundisha.