Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 5

Busara

Busara

Kanuni: “Maneno yenu yakuwe yenye kupendeza sikuzote.”​—Kol. 4:6.

Mambo Yenye Paulo Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 17:22, 23. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Paulo alijisikia namna gani juu ya matendo ya watu wa madini ya uongo kule Atene?​—Ona Matendo 17:16.

  2.   Kuliko kuwahukumu, namna gani Paulo alizungumuza nao kwa busara wakati alitumia mambo yenye waliamini juu ya kuwahubiria habari njema?

Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?

2. Kama tunachagua muzuri mambo yenye tutasema, namna tutaisema, na wakati tutaisema, watu wanaweza kufurahia kutusikiliza.

Umuige Paulo

3. Chagua maneno muzuri. Kwa mufano, wakati unaongea na mutu mwenye iko mu dini yenye haiko ya Kikristo, inaweza kuwa muzuri kubadilisha namna utatanguliza andiko ao mambo yenye utasema juu ya Yesu.

4. Usikuwe haraka kurekebisha mutu. Umuache ajieleze waziwazi bila kumukatiza. Kama anasema jambo fulani yenye haipatane na mafundisho ya Biblia, uepuke kabisa kubishana naye. (Yak. 1:19) Kama unamusikiliza njo utafikia kujua mawazo yenye kuwa ndani ya moyo wake.​—Mez. 20:5.

5. Kama inafaa, ukubali mawazo yake na umupongeze. Pengine iko hakika kama mambo yenye anaamini njo ya kweli. Ku mwanzo, uzungumuzie kwanza mambo yenye nyiye wote munaamini. Polepole njo utamusaidia kuelewa mambo yenye Biblia inafundisha.