Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 6

Ujasiri

Ujasiri

Kanuni: “Mungu wetu alitufanya tusikuwe na woga ili tuwatangazie ninyi habari njema.”​—1 Tes. 2:2.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Luka 19:1-7. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Ni mambo gani yenye ingefanya watu waogope kumukaribia Zakayo?

  2.   Hata vile, nini njo ilifanya Yesu aende kumuhubiria?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Tuko na lazima ya ujasiri juu tuhubirie watu bila kuwabagua.

Umuige Yesu

3. Umutumainie Yehova. Vile tu roho ya Mungu ilimupatia Yesu nguvu ya kuhubiri, inaweza pia kukupatia na weye nguvu. (Mt. 10:19, 20; Lu. 4:18) Umuombe Yehova akusaidie ukuwe na ujasiri juu uhubirie watu wenye wanaweza kukuogopesha​—Mdo. 4:29.

4. Usikuwe haraka kuhukumu mutu. Unaweza kuogopa kuhubiria mutu pengine juu ya namna anaonekana kwa inje, juu iko tajiri, juu ya tabia yake, ao juu ya mambo yenye anaamini. Lakini kumbuka hii mambo:

  1.    Yehova na Yesu njo wako na uwezo wa kusoma mioyo ya watu; siye hatuna ile uwezo.

  2.   Yehova anaweza kusaidia mutu yeyote mwenye anapenda.

5. Ukuwe na ujasiri, lakini pia ukuwe na heshima na ukuwe muangalifu. (Mt. 10:16) Usibishane. Wakati unaona kama uko mu hatari ao mutu hapendi kusikiliza habari njema, kwa heshima unaweza kusimamisha mazungumuzo.​—Mez. 17:14.