KUANZISHA MAZUNGUMZO

SOMO LA 6

Ujasiri

Ujasiri

Kanuni: “Tulijipa ujasiri kupitia Mungu wetu ili tuwatangazie ninyi habari njema ya Mungu.”—1 The. 2:2.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Luka 19:​1-7. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Kwa nini baadhi ya watu waliepuka kushirikiana na Zakayo?

  2.   Ni nini kilichomchochea Yesu amhubirie habari njema?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunahitaji ujasiri ili tuhubiri ujumbe wa Ufalme bila ubaguzi.

Mwige Yesu

3. Mtegemee Yehova. Roho ya Mungu ilimpa Yesu nguvu za kuhubiri, na inaweza kukusaidia pia. (Mt. 10:​19, 20; Luka 4:18) Mwombe Yehova akupe ujasiri wa kuwahubiria watu unaowaogopa.—Mdo. 4:29.

4. Usiwahukumu watu. Huenda tukasita kuzungumza na baadhi ya watu kwa sababu ya mwonekano wao, cheo chao katika jamii au hali yao ya kiuchumi, mtindo wao wa maisha, au dini yao. Lakini kumbuka:

  1.    Yehova na Yesu wanaweza kusoma mioyo; sisi hatuwezi.

  2.   Tusihisi kwamba mtu huyo hawezi kusaidiwa na Yehova.

5. Uwe jasiri lakini mwenye busara na tahadhari. (Mt. 10:16) Epuka kubishana. Maliza mazungumzo kwa upole ikiwa mtu hataki kusikiliza habari njema au unahisi hauko salama.—Met. 17:14.