KUENDELESHA MAZUNGUMUZO
SOMO YA 7
Kutovunjika Moyo
Kanuni: “Wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema.”—Mdo. 5:42.
Mambo Yenye Paulo Alifanya
1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 19:8-10. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:
Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?
2. Inaombaka wakati na kujikaza sana juu tupate matokeo ya muzuri wakati tunarudilia watu na wakati tunaanzisha mafunzo ya Biblia.
Umuige Paulo
3. Patanisha programu yako na ya mutu mwenye unahubiria. Ujiulize hivi: ‘Ni wakati gani njo anaweza kufurahia nimutembelee? Ni wakati gani na wapi njo atapenda tuzungumuze naye?’ Ukuwe tayari kumutembelea ile wakati, hata kama haipatane na programu yako.
4. Mupange wakati ya kuonana tena. Ku mwisho wa kila mazungumuzo, mujikaze kupanga siku na saa yenye mutakutana tena. Ufanye yako yote ili uheshimie ile programu.
5. Usivunjike moyo. Usiwaze mara moya kama juu tu haumupatake ule mutu ao juu anakuwaka na mambo mingi ya kufanya maana yake hapendezwe. (1 Ko. 13:4, 7) Kuliko kuwaza vile, ujikaze kuendelea kumutembelea, bila kusahau kama unapaswa kutumia wakati yako kwa hekima.—1 Ko. 9:26.