KUFUATIA UPENDEZI

SOMO LA 7

Uvumilivu

Uvumilivu

Kanuni: “Wakaendelea kufundisha na kutangaza habari njema . . . bila kuacha.”—Mdo. 5:42.

Paulo Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Matendo 19:​8-10. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Badala ya kukata tamaa wengine walipompinga, Paulo alionyeshaje uvumilivu alipowasaidia watu waliopendezwa?

  2.   Ni mara ngapi Paulo alirudi kuwafundisha watu waliopendezwa, na alifanya hivyo kwa muda gani?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Paulo?

2. Tunahitaji kutumia wakati na jitihada ili kufanya ziara za kurudia zenye matokeo mazuri na kuanzisha mafunzo ya Biblia.

Mwige Paulo

3. Badili ratiba yako ipatane na ya mtu huyo. Jiulize hivi: ‘Ni wakati gani unaomfaa nitakaoweza kuonana naye? Ni lini atakuwa na nafasi na tutakutana wapi ili tuendeleze mazungumzo yetu?’ Uwe tayari kumtembelea hata ikiwa si wakati unaokufaa.

4. Weka ahadi ya kuzungumza naye tena. Unapomalizia mazungumzo, jaribu kupanga wakati hususa mtakaozungumza tena na mtu huyo. Hakikisha kwamba unatimiza ahadi yako.

5. Usife moyo. Usifikiri kwamba mtu hapendezwi kwa sababu si rahisi kumpata nyumbani au ana shughuli nyingi sana. (1 Kor. 13:​4, 7) Badala yake, endelea kumtafuta mtu huyo, lakini hakikisha kwamba unatumia vizuri wakati wako.—1 Kor. 9:26.