Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

KUFUATIA UPENDEZI

SOMO LA 8

Subira

Subira

Kanuni: “Upendo ni wenye subira.”—1 Kor. 13:4.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 7:​3-5 na 1 Wakorintho 15:​3, 4, 7. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Mwanzoni, ndugu za Yesu waliitikiaje alipowahubiria?

  2.   Ni nini kinachoonyesha kwamba Yesu aliendelea kumsaidia ndugu yake Yakobo?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunahitaji kuwa na subira kwa sababu baadhi ya watu hawakubali haraka habari njema.

Mwige Yesu

3. Jaribu kutumia njia nyingine. Ikiwa mtu hakubali mara moja kujifunza Biblia, usimlazimishe. Inapofaa, tumia video au makala fulani kumsaidia aelewe kinachotendeka kwenye funzo la Biblia na jinsi atakavyonufaika.

4. Usimlinganishe na wengine. Watu wanatofautiana. Ikiwa mshiriki wa familia au mtu unayemrudia anasita kujifunza Biblia au kukubali fundisho la Biblia, fikiria kwa nini anafanya hivyo. Je, kuna fundisho la dini analopenda sana? Je, anashinikizwa na watu wa ukoo au majirani? Mpe muda wa kufikiria mambo uliyomwambia na kuthamini mafundisho ya Biblia.

5. Sali kwa ajili ya watu wanaopendezwa. Mwombe Yehova akusaidie uwe na busara na mtazamo mzuri. Sali ili utambue ni wakati gani unapaswa kuacha kumtembelea tena mtu ambaye hapendezwi.—1 Kor. 9:26.