Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUENDELESHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 8

Uvumilivu

Uvumilivu

Kanuni: “Upendo ni wenye uvumilivu.”​—1 Ko. 13:4.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Yohana 7:3-5 na 1 Wakorinto 15:3, 4, 7. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Ku mwanzo, namna gani ndugu za Yesu walipokea ujumbe wake?

  2.   Nini njo inaonyesha kama Yesu aliendelea kumusaidia ndugu yake Yakobo?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Inaomba tukuwe wavumilivu juu watu fulani hawaitikake habari njema haraka.

Umuige Yesu

3. Tumikisha njia zingine. Kama mutu hakubali mara moya funzo ya Biblia, usimukaze. Kwa wakati wenye kufaa, tumikisha mavideo ao habari fulani zenye zitamusaidia ajue namna funzo ya Biblia inafanyikaka na namna inaweza kumusaidia.

4. Usilinganishe watu. Kila mutu iko namna yake. Kama mutu fulani wa familia ao mutu mwenye unarudilia iko nasita kukubali funzo ya Biblia ao kuamini kweli fulani ya Biblia, ujikaze kujua ni juu ya nini. Inawezekana pengine anapendaka sana fundisho fulani ya dini? Ao pengine ni juu watu fulani wa familia ao majirani wako namuchekelea na kumukaza aache kujifunza? Umuachie wakati juu afikirie mambo fulani yenye mumezungumuzia na aone faida ya kujifunza Biblia.

5. Sali juu ya mutu mwenye kupendezwa. Umuombe Yehova akusaidie usivunjike moyo. Umuombe pia akusaidie ujue ni wakati gani njo unaweza kuacha kumutembelea mutu mwenye hapendezwe sana.​—1 Ko. 9:26.