KUFUATIA UPENDEZI
SOMO LA 9
Huruma
Kanuni: “Shangilieni na wale wanaoshangilia; lieni na wale wanaolia.”—Rom. 12:15.
Yesu Alifanya Nini?
1. Tazama VIDEO, au soma Marko 6:30-34. Kisha fikiria maswali yafuatayo:
Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
2. Huruma inatuchochea kuwajali watu, si kuwaambia tu ujumbe wetu.
Mwige Yesu
3. Sikiliza kwa makini. Mruhusu mtu unayezungumza naye ajieleze. Usimkatishe au kupuuza hisia zake, mahangaiko yake au mambo asiyokubaliana nayo. Kwa kumsikiliza kwa makini, utaonyesha kwamba unajali mambo anayosema.
4. Mfikirie mtu anayependezwa. Ikitegemea mazungumzo yako, jiulize hivi:
5. Zungumzia mambo yanayoweza kumsaidia. Bila kukawia, mwonyeshe jinsi ambavyo kujifunza Biblia kunaweza kujibu maswali yake na kumsaidia katika njia hususa.