Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUENDELESHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 9

Kujitia pa Nafasi ya Mutu

Kujitia pa Nafasi ya Mutu

Kanuni: “Mufurahi pamoja na wale wenye kufurahi; mulie pamoja na wale wenye kulia.”​—Ro. 12:15.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Marko 6:30-34. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Juu ya nini Yesu na wanafunzi wake walipenda ‘kuwa peke yao’?

  2.   Nini njo ilifanya Yesu afundishe wale watu wengi sana?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Kujitia pa nafasi ya wengine kunafanya tuwahangaikie kuliko tu kuhangaikia ujumbe wetu.

Umuige Yesu

3. Sikiliza kwa uangalifu. Umuache musikilizaji aseme mambo yenye iko namuhangaisha. Usimukatize wakati iko nasema, na usizarau mambo yenye inamuhangaisha, ao mambo yenye anasema yenye haipatane na yetu. Kama unamusikiliza kwa uangalifu, utaonyesha kama unaheshimia mawazo yake.

4. Ukuwe nawaza juu ya mutu mwenye alipendezwa. Fikiria juu ya mambo yenye ulizungumuza naye, na ujiulize hivi:

  1.    ‘Juu ya nini huyu mutu iko na lazima ya kusikia kweli?’

  2.   ‘Namna gani kujifunza Biblia kunaweza kufanya maisha yake ikuwe muzuri leo na wakati yenye kuya?’

5. Muzungumuzie mambo yenye inaweza kumusaidia. Bila kukawia, umuonyeshe namna funzo ya Biblia inaweza kumusaidia apate majibu ya maulizo yenye anajiulizaka na namna inaweza kumusaidia mu mambo ingine.