KUFUATIA UPENDEZI

SOMO LA 9

Huruma

Huruma

Kanuni: “Shangilieni na wale wanaoshangilia; lieni na wale wanaolia.”—Rom. 12:15.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Marko 6:​30-34. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Kwa nini Yesu na mitume wake walitarajia ‘kuwa peke yao’?

  2.   Ni nini kilichomchochea Yesu aufundishe umati?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Huruma inatuchochea kuwajali watu, si kuwaambia tu ujumbe wetu.

Mwige Yesu

3. Sikiliza kwa makini. Mruhusu mtu unayezungumza naye ajieleze. Usimkatishe au kupuuza hisia zake, mahangaiko yake au mambo asiyokubaliana nayo. Kwa kumsikiliza kwa makini, utaonyesha kwamba unajali mambo anayosema.

4. Mfikirie mtu anayependezwa. Ikitegemea mazungumzo yako, jiulize hivi:

  1.    ‘Kwa nini anahitaji kusikia kweli?’

  2.   ‘Kujifunza Biblia kutaboreshaje maisha yake ya sasa na ya wakati ujao?’

5. Zungumzia mambo yanayoweza kumsaidia. Bila kukawia, mwonyeshe jinsi ambavyo kujifunza Biblia kunaweza kujibu maswali yake na kumsaidia katika njia hususa.