Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

KUFANYA WANAFUNZI

SOMO LA 10

Azimia Kuwasaidia Watu Wawe Wanafunzi

Azimia Kuwasaidia Watu Wawe Wanafunzi

Kanuni: “Tulijitahidi kuwapa habari njema ya Mungu na hata uhai wetu wenyewe, kwa sababu tuliwapenda sana.”—1 The. 2:8.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 3:​1, 2. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Kwa nini Nikodemo alimtembelea Yesu usiku? —Ona Yohana 12:​42, 43.

  2.   Kwa kukutana na Nikodemo usiku, Yesu alionyeshaje kwamba aliazimia kufanya wanafunzi?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Kwa sababu tunawapenda watu, tumeazimia kuwasaidia wawe wanafunzi.

Mwige Yesu

3. Jifunze na mwanafunzi wa Biblia kwa wakati na mahali panapomfaa. Anaweza kupendekeza siku fulani katika juma au wakati hususa wa kujifunza. Je, anafurahia kujifunza akiwa kazini, nyumbani au katika eneo fulani la umma? Badili ratiba yako kadiri iwezekanavyo ili ipatane na mahitaji ya mwanafunzi.

4. Mjifunze kwa ukawaida. Ikiwa utasafiri, usisitishe ratiba yenu ya kujifunza. Badala yake, fikiria mambo yafuatayo:

  1.    Je, unaweza kuongoza funzo siku nyingine katika juma hilo?

  2.   Je, unaweza kuongoza funzo kupitia simu au video?

  3.   Je, unaweza kumwomba mhubiri mwingine aongoze funzo?

5. Sali ili uwe na mtazamo mzuri. Mwombe Yehova akusaidie uendelee kuazimia kumsaidia mwanafunzi wako, hata ikiwa si rahisi kwake kujifunza kwa ukawaida au anachukua muda mrefu kutumia ushauri wa Maandiko. (Flp. 2:13) Huenda mwanafunzi wako ana sifa nyingi nzuri; sali kwa Yehova akusaidie uzingatie sifa hizo.