Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUFANYA WANAFUNZI

SOMO YA 11

Kufundisha mu Njia ya Mwepesi

Kufundisha mu Njia ya Mwepesi

Kanuni: ‘Museme . . . maneno yenye kueleweka kwa urahisi.’​—1 Ko. 14:9.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Matayo 6:25-27. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Namna gani Yesu alionyesha kama Yehova anatuhangaikiaka?

  2.   Hata kama Yesu alijua mambo mingi juu ya ndege, alikazia maelezo gani ya mwepesi mu mufano wake? Juu ya nini tunaweza kusema kama ile njia ya kufundisha ilikuwa ya muzuri?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Wakati tunafundisha mu njia ya mwepesi, watu watakumbuka mambo yenye tuliwafundisha na tutagusa mioyo yao.

Umuige Yesu

3. Usiseme mingi. Kuliko kusema yote yenye unajua juu ya habari, zungumuzia mambo yenye iko mu kichapo yenye muko najifunza. Kisha kuuliza ulizo, uchunge mwanafunzi wako ajibie. Kama hajue jibu ao kama jibu yake haipatane na mafundisho ya Biblia, tumia maulizo ingine juu ya kumusaidia afikie kupata jibu. Kama tu mwanafunzi alishaelewa wazo kubwa, mupite ku jambo yenye kufuata.

4. Saidia mwanafunzi wako apatanishe mafundisho ya mupya na ile yenye alishajua. Kwa mufano, mbele ya kuanza kuzungumuzia somo yenye inahusu ufufuo, unaweza kurudilia kwa kifupi mambo yenye mwanafunzi alishajifunza kuhusu hali ya watu wenye walishakufa.

5. Tumia muzuri mifano. Mbele ya kutoa mufano, ujiulize hivi:

  1.    ‘Hii mufano iko ya mwepesi?’

  2.   ‘Mwanafunzi anaweza kuielewa bila magumu?’

  3.   ‘Itamusaidia akumbuke habari kubwa, kuliko tu kukumbuka mufano?’