Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUFANYA WANAFUNZI

SOMO YA 12

Uhodari

Uhodari

Kanuni: “Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo, ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.”​—Mez. 27:9.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Marko 10: 17-22. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Pengine Yesu aliona sifa gani za muzuri kwa ule mutawala kijana?

  2.   Juu ya nini iliomba Yesu akuwe na upendo na uhodari juu amushaurie ule kijana?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Juu mutu afanye maendeleo ya kiroho, ni kweli tunapaswa kuzungumuza naye kwa upendo; lakini tunapaswa pia kuzungumuza naye waziwazi, ikiwa inaomba afanye mabadiliko fulani.

Umuige Yesu

3. Saidia mwanafunzi ajiwekee miradi na kuitimiza.

  1.    Tumikisha sehemu “Pima Kufanya Hivi” mu kila somo ya kitabu Furahia Maisha Milele!

  2.   Saidia mwanafunzi wako ajue mambo yenye anapaswa kufanya juu atimize miradi ya wakati mufupi na ya wakati murefu.

  3.   Kila mara umupongeze juu ya maendeleo yenye iko nafanya.

4. Tambua magumu yenye inazuia mwanafunzi wako kufanya maendeleo na umusaidie aipiganishe.

  1.    Ujiulize hivi:

    • ‘Kama hafanye maendeleo juu afikie kubatizwa, pengine nini njo iko namuzuia?’

    • ‘Naweza kufanya nini juu ya kumusaidia?’

  2.   Umuombe Yehova akupatie uhodari juu uzungumuze naye waziwazi na kwa upendo kuhusu mabadiliko yenye anapaswa kufanya.

5. Kama mwanafunzi hafanye maendeleo, musimamishe funzo.

  1.    Unaweza kujua kama mwanafunzi hafanye maendeleo kwa kujiuliza hii maulizo:

    • ‘Huyu mwanafunzi anatumikishaka mambo yenye iko najifunza?’

    • ‘Anaendaka ku mikutano na kuambia watu wengine mambo yenye iko najifunza?’

    • ‘Kisha kujifunza naye kwa wakati fulani, anaonyesha kama anapenda kuwa Shahidi wa Yehova?’

  2.   Kama mwanafunzi wa Biblia hapendi kufanya maendeleo ya kiroho:

    • Umuambie afikirie mambo yenye iko namuzuia.

    • Kwa heshima umuambie juu ya nini unapenda musimamishe funzo.

    • Umuambie maendeleo yenye anapaswa kufanya juu muanze tena kujifunza.