KUFANYA WANAFUNZI

SOMO LA 12

Uhodari

Uhodari

Kanuni: “Mafuta na uvumba huufanya moyo ushangilie; ndivyo ulivyo urafiki mtamu unaochipuka kutokana na shauri la unyoofu.”—Met. 27:9.

Yesu Alifanya Nini?

1. Tazama VIDEO, au soma Marko 10:​17-22. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1.    Huenda Yesu aliona sifa gani nzuri za mtawala kijana?

  2.   Kwa nini Yesu alihitaji upendo na uhodari ili kumshauri mwanamume huyo?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunahitaji kuzungumza kwa upendo lakini tuwaeleze waziwazi wanafunzi wetu mambo yatakayowasaidia kufanya maendeleo ya kiroho.

Mwige Yesu

3. Msaidie mwanafunzi aweke malengo na kuyafikia.

  1.    Tumia sehemu ya “Lengo” katika kila somo la kitabu Furahia Maisha Milele!

  2.   Msaidie mwanafunzi aelewe mambo anayopaswa kufanya ili afikie malengo ya muda mfupi na ya muda mrefu.

  3.   Mpongeze mwanafunzi kwa ukawaida kwa maendeleo anayofanya.

4. Unahitaji kujua hali zinazomzuia mwanafunzi wako kufanya maendeleo na umsaidie ashinde hali hizo.

  1.    Jiulize hivi:

    • ‘Ni nini kinachomzuia mwanafunzi wangu kufanya maendeleo kufikia ubatizo?’

    • ‘Ninawezaje kumsaidia?’

  2.   Sali upate uhodari wa kuzungumza na mwanafunzi wako kwa upendo lakini waziwazi kuhusu mambo anayohitaji kufanya.

5. Sitisha funzo ikiwa mwanafunzi hafanyi maendeleo.

  1.    Changanua ikiwa mwanafunzi anafanya maendeleo kwa kujiuliza hivi:

    • ‘Je, mwanafunzi wangu anatumia mambo anayojifunza?’

    • ‘Je, anahudhuria mikutano ya kutaniko na kuwahubiria wengine kuhusu kweli anazojifunza?’

    • ‘Baada ya kujifunza kwa muda fulani, je, anataka kuwa Shahidi wa Yehova?’

  2.   Ikiwa mwanafunzi wa Biblia hayuko tayari kufanya maendeleo:

    • Mwombe afikirie kuhusu jambo linalomzuia kufanya maendeleo.

    • Kwa fadhili, mweleze kwa nini unaacha kujifunza naye Biblia.

    • Mweleze maendeleo anayohitaji kufanya kabla ya kuanza kujifunza naye tena.