Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

NYONGEZA A

Kweli Tunazopenda Kufundisha

Kweli Tunazopenda Kufundisha

Yesu alisema watu wenye mioyo minyoofu watatambua kweli wanapoisikia. (Yoh. 10:​4, 27) Kwa hiyo, kila tunapozungumza na watu tunahitaji kuwaeleza kweli rahisi zinazopatikana katika Biblia. Jaribu kuanza kwa kuuliza hivi: “Je, unajua kwamba . . . ?” au “Umewahi kusikia kwamba . . . ?” Kisha tumia Biblia kufafanua kweli hiyo. Kweli rahisi ya Biblia inaweza kupanda mbegu katika moyo wa mtu, na Mungu anaweza kuikuza mbegu hiyo!—1 Kor. 3:​6, 7.

 WAKATI UJAO

  1. 1. Matukio tunayoona na jinsi watu wanavyojiendesha, ni ishara ya kwamba hivi karibuni hali zitabadilika.—Mt. 24:​3, 7, 8; Luka 21:​10, 11; 2 Tim. 3:​1-5.

  2. 2. Dunia haitaharibiwa kamwe.—Zab. 104:5; Mhu. 1:4.

  3. 3. Mazingira yatakuwa bora na dunia itakuwa paradiso.—Isa. 35:​1, 2; Ufu. 11:18.

  4. 4. Kila mtu atakuwa na afya kamilifu.—Isa. 33:24; 35:​5, 6.

  5. 5. Unaweza kuishi milele duniani.—Zab. 37:29; Mt. 5:5.

 FAMILIA

  1. 6. Mume anapaswa “kumpenda mke wake kama anavyojipenda mwenyewe.”—Efe. 5:33; Kol. 3:19.

  2. 7. Mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.—Efe. 5:33; Kol. 3:18.

  3. 8. Mume na mke wanapaswa kuwa waaminifu.—Mal. 2:16; Mt. 19:​4-6, 9; Ebr. 13:4.

  4. 9. Watoto wanaowaheshimu na kuwatii wazazi wao watafanikiwa.—Met. 1:​8, 9; Efe. 6:​1-3.

NASA, ESA and the Hubble Heritage Team (STScI/AURA)-ESA/Hubble Collaboration. Licensed under CC BY 4.0. Source.

 MUNGU

  1. 10. Mungu ana jina.—Zab. 83:18; Yer. 10:10.

  2. 11. Mungu anawasiliana nasi.—2 Tim. 3:​16, 17; 2 Pet. 1:​20, 21.

  3. 12. Mungu hana ubaguzi na anatenda kwa haki.—Kum. 10:17; Mdo. 10:​34, 35.

  4. 13. Mungu anataka kutusaidia.—Zab. 46:1; 145:​18, 19.

 SALA

  1. 14. Mungu anataka tusali kwake.—Zab. 62:8; 65:2; 1 Pet. 5:7.

  2. 15. Biblia inatufundisha jinsi ya kusali.—Mt. 6:​7-13; Luka 11:​1-4.

  3. 16. Tunapaswa kusali mara nyingi.—Mt. 7:​7, 8; 1 The. 5:17.

 YESU

  1. 17. Yesu ni mwalimu mkuu na sikuzote ushauri wake unafaa.—Mt. 6:​14, 15, 34; 7:12.

  2. 18. Yesu alitabiri matukio tunayoona leo.—Mt. 24:​3, 7, 8, 14; Luka 21:​10, 11.

  3. 19. Yesu ni Mwana wa Mungu. —Mt. 16:16; Yoh. 3:16; 1 Yoh. 4:15.

  4. 20. Yesu si Mungu Mweza Yote.—Yoh. 14:28; 1 Kor. 11:3.

Based on NASA/Visible Earth imagery

 UFALME WA MUNGU

  1. 21. Ufalme wa Mungu ni serikali halisi iliyo mbinguni.—Dan. 2:44; 7:​13, 14; Mt. 6:​9, 10; Ufu. 11:15.

  2. 22. Ufalme wa Mungu utaondoa serikali za wanadamu.—Zab. 2:​7-9; Dan. 2:44.

  3. 23. Ufalme wa Mungu ndio suluhisho pekee la matatizo ya wanadamu.—Zab. 37:​10, 11; 46:9; Isa. 65:​21-23.

 KUTESEKA

  1. 24. Mungu hasababishi mateso tunayokabili.—Kum. 32:4; Yak. 1:13.

  2. 25. Shetani anautawala ulimwengu huu.—Luka 4:​5, 6; 1 Yoh. 5:19.

  3. 26. Mungu anaona unapoteseka na anataka kukusaidia.—Zab. 34:​17-19; Isa. 41:​10, 13.

  4. 27. Hivi karibuni Mungu atakomesha mateso.—Isa. 65:17; Ufu. 21:​3, 4.

 KIFO

  1. 28. Wafu hawajui jambo lolote wala hawateseki.—Mhu. 9:5; Yoh. 11:​11-14.

  2. 29. Wafu hawawezi kutusaidia au kutuumiza.—Zab. 146:4; Mhu. 9:​6, 10.

  3. 30. Wapendwa wetu waliokufa watafufuliwa.—Ayu. 14:​13-15; Yoh. 5:​28, 29; Mdo. 24:15.

  4. 31. “Kifo hakitakuwapo tena.”—Ufu. 21:​3, 4; Isa. 25:8.

 DINI

  1. 32. Si dini zote zinazompendeza Mungu.—Yer. 7:11; Mt. 7:​13, 14, 21-23.

  2. 33. Mungu anachukia unafiki.—Isa. 29:13; Mika 3:11; Marko 7:​6-8.

  3. 34. Upendo wa kweli hutambulisha dini ya kweli.—Mika 4:3; Yoh. 13:​34, 35.