Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NYONGEZA YA A

Kweli Zenye Tunapendaka Kufundisha

Kweli Zenye Tunapendaka Kufundisha

Yesu alisema kama watu wenye mioyo mizuri wakisikia tu kweli watajua kama hii ni kweli. (Yoh. 10:4, 27) Njo maana wakati tuko nazungumuza na mutu, ni muzuri tumuambie tu kweli za Biblia za mwepesi. Uambie mutu kweli fulani ya Biblia kwa kumuuliza tu: “Unajuaka kama . . . ?” ao “Ulishakasikia kama . . . ?” Kisha utumikishe andiko ao maandiko yenye inapatana na ile kweli juu ya kuifasiria. Ile tu kuambia mutu kweli fulani ya Biblia inaweza kuwa kupanda mbegu mu moyo wake, na Mungu anaweza kuikomalisha!​—1 Ko. 3:6, 7.

 WAKATI WENYE KUYA

  1. 1. Mambo yenye iko nafanyika leo na matendo ya batu inaonyesha kama mwisho uko karibu.​—Mt. 24:3, 7, 8; Lu. 21:10, 11; 2 Ti. 3:1-5.

  2. 2. Hii dunia haitaharibiwaka.​—Zb. 104:5; Muh. 1:4.

  3. 3. Hii dunia itasafishiwaka na kukuwa tena paradiso.​—Isa. 35:1, 2; Ufu. 11:18.

  4. 4. Kila mutu atakuwaka na afya ya muzuri.​—Isa. 33:24; 35:5, 6.

  5. 5. Unaweza kuishi milele ku dunia.​—Zb. 37:29; Mt. 5:5.

 FAMILIA

  1. 6. Bwana anapaswa kupenda bibi yake vile anajipendaka yeye mwenyewe.​—Efe. 5:33; Kol. 3:19.

  2. 7. Bibi anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.​—Efe. 5:33; Kol. 3:18.

  3. 8. Bwana anapaswa kuwa muaminifu kwa bibi yake na bibi anapaswa kuwa muaminifu kwa bwana yake.​—Mal. 2:16; Mt. 19:4-6, 9; Ebr. 13:4.

  4. 9. Batoto benye kuheshimia na kutii bazazi njo banakuwaka na maisha ya muzuri.​—Mez. 1:8, 9; Efe. 6:1-3.

NASA, ESA and the Hubble Heritage Team (STScI/​AURA)-ESA/​Hubble Collaboration. Licensed under CC BY 4.0. Source.

 MUNGU

  1. 10. Mungu anakuwaka na jina.​—Zb. 83:18; Yer. 10:10.

  2. 11. Mungu anaongeaka na siye.​—2 Ti. 3:16, 17; 2 Pe. 1:20, 21.

  3. 12. Mungu anatendeaka batu yote sawasawa na hakuwake na ubaguzi.​—Kum. 10:17; Mdo. 10:34, 35.

  4. 13. Mungu anapenda kutusaidia.​—Zb. 46:1; 145:18, 19.

 SALA

  1. 14. Mungu anapenda tusali kwake.​—Zb. 62:8; 65:2; 1 Pe. 5:7.

  2. 15. Biblia inatufundisha namna ya kusali.​—Mt. 6:7-13; Lu. 11:1-4.

  3. 16. Tunapaswa kusali kila mara.​—Mt. 7:7, 8; 1 Te. 5:17.

 YESU

  1. 17. Yesu alikuwaka mwalimu mukubwa, na mashauri yake inasaidiaka kila mara.​—Mt. 6:14, 15, 34; 7:12.

  2. 18. Yesu alizungumuziaka mambo yenye tuko naona leo.​—Mt. 24:3, 7, 8, 14; Lu. 21:10, 11.

  3. 19. Yesu ni Mutoto wa Mungu.​—Mt. 16:16; Yoh. 3:16; 1 Yo. 4:15.

  4. 20. Yesu haiko Mungu Mweza-yote.​—Yoh. 14:28; 1 Ko. 11:3.

Based on NASA/​Visible Earth imagery

 UFALME WA MUNGU

  1. 21. Ufalme wa Mungu ni guvernema ya kwelikweli yenye iko mbinguni.​— Da. 2:44; 7:13, 14; Mt. 6:9, 10; Ufu. 11:15.

  2. 22. Ufalme wa Mungu utakamata nafasi ya guvernema za wanadamu.​—Zb. 2:7-9; Da. 2:44.

  3. 23. Ufalme wa Mungu tu njo wenye utamaliza magumu ya wanadamu.​—Zb. 37:10, 11; 46:9; Isa. 65:21-23.

 MATESO

  1. 24. Haiko Mungu njo anatuleteaka mateso.​—Kum. 32:4; Yak. 1:13.

  2. 25. Shetani njo iko natawala hii dunia.​—Lu. 4:5, 6; 1 Yo. 5:19.

  3. 26. Mungu anaonaka mateso yako na anapenda kukusaidia.​—Zb. 34:17-19; Isa. 41:10, 13.

  4. 27. Mungu atamaliza mateso hivi karibuni.​—Isa. 65:17; Ufu. 21:3, 4.

 KIFO

  1. 28. Benye balishakufa habajuake kitu na habatesekake.​—Muh. 9:5; Yoh. 11:11-14.

  2. 29. Benye balishakufa habawezi kutusaidia ao kututendea mubaya.​—Zb. 146:4; Muh. 9:6, 10.

  3. 30. Batu benye tulikuwa napenda benye balishakufa batafufukaka.​—Yob. 14:13-15; Yoh. 5:28, 29; Mdo. 24:15.

  4. 31. “Kifo hakitakuwa tena.”​—Ufu. 21:3, 4; Isa. 25:8.

 DINI

  1. 32. Haiko madini yote njo inamufurahishaka Mungu.​—Yer. 7:11; Mt. 7:13, 14, 21-23.

  2. 33. Mungu anachukiaka unafiki.​—Isa. 29:13; Mik. 3:11; Mk. 7:6-8.

  3. 34. Upendo wa kweli njo unatusaidia kujua dini ya kweli.​—Mik. 4:3; Yoh. 13:34, 35.