Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NYONGEZA YA C

Namna ya Kuongoza Funzo ya Biblia kwa Kutumia Furahia Maisha Milele!

Namna ya Kuongoza Funzo ya Biblia kwa Kutumia Furahia Maisha Milele!

Juu kitabu Furahia Maisha Milele! itolewe, ndugu walisali na kuchunguza sana habari zenye wangetia ndani. Njo maana, juu utumikishe muzuri hii kitabu, fuata mashauri yenye kuwa hapa chini wakati uko naongoza mafunzo ya Biblia.

Mbele ya funzo

  1. 1. Ujitayarishe sana. Wakati uko nafanya vile, ufikirie mahitaji, hali, na mawazo ya mwanafunzi. Pima kuwazia mbele ya wakati mambo yenye pengine mwanafunzi hataelewa mbiombio. Fikiria namna mawazo yenye kuwa mu sehemu ”‏Habari Zingine”‏ inaweza kusaidia mwanafunzi na ukuwe tayari kuitumikisha wakati wa funzo, kama ni lazima.

Wakati wa funzo

  1. 2. Kama mwanafunzi wako anakubali, muanze na sala na mumalize na sala.

  2. 3. Ukuwe muangalifu usiseme mingi. Ukazie mawazo yenye kuwa mu kichapo na uache mwanafunzi ajieleze.

  3. 4. Ku mwanzo wa kila sehemu, uzungumuzie wazo kubwa ya ile sehemu na uzungumuzie somo fulani zenye kuwa ndani.

  4. 5. Wakati munamaliza sehemu fulani, uulize maulizo ya kujikumbusha ya ile sehemu juu ya kumusaidia mwanafunzi akumbuke kweli zenye amejifunza mu ile sehemu.

  5. 6. Wakati uko najifunza kila somo na mwanafunzi:

    1. Musome mafungu.

    2. Musome maandiko yote yenye inatangulizwa na neno “Soma.”

    3. Musome maandiko ingine yenye inaweza kusaidia.

    4. Muangalie mavideo yenye inatangulizwa na neno “Muangalie” (kama inawezekana).

    5. Uliza mwanafunzi kila ulizo.

    6. Umuombe mwanafunzi aangalie mapicha yenye kuwa ku sehemu “Tujifunze Mambo Mingi Zaidi” na umuambie atoe maelezo fulani juu ya ile mapicha.

    7. Tumikisha sehemu “Pima Kufanya Hivi” juu ya kusaidia mwanafunzi afanye maendeleo ya kiroho. Utie moyo mwanafunzi atumikishe pendekezo yenye kuwa ku ile sehemu ao afikirie jambo ingine yenye anaweza kufanya, ao byote biwili.

    8. Umuulize mwanafunzi ikiwa kuko video ao habari fulani yenye ilimufurahisha wakati alikuwa natayarisha sehemu “Habari Zingine.”

    9. Mujikaze kumaliza somo kila mara wakati munajifunza.

Kisha funzo

  1. 7. Uendelee kuwaza juu ya mwanafunzi wako. Umuombe Yehova amusaidie afanye maendeleo na umuombe akupatie hekima juu ujue namna ya kumusaidia.