NYONGEZA C

Jinsi ya Kuongoza Mafunzo ya Biblia kwa Kutumia Kitabu Furahia Maisha Milele!

Jinsi ya Kuongoza Mafunzo ya Biblia kwa Kutumia Kitabu Furahia Maisha Milele!

Ndugu walisali sana na wakafanya utafiti mwingi ili kutayarisha chapisho la Furahia Maisha Milele! Ili uweze kutumia kikamili chapisho hilo, fuata madokezo yafuatayo unapoongoza mafunzo ya Biblia.

Kabla ya funzo

  1. 1. Tayarisha somo vizuri. Unapofanya hivyo, fikiria mahitaji, hali, na maoni ya mwanafunzi wako. Wazia mambo yoyote ambayo huenda ni vigumu kwake kuelewa au kutumia. Tafakari jinsi habari zilizo katika sehemu ya “Chunguza Zaidi” zinavyoweza kumsaidia mwanafunzi wako, na uwe tayari kuzitumia wakati wa funzo kulingana na mahitaji yake.

Wakati wa funzo

  1. 2. Sali kabla na baada ya funzo ikiwa mwanafunzi wako anakubali.

  2. 3. Usizungumze kupita kiasi. Kazia habari mnayozungumzia, na mruhusu mwanafunzi ajieleze.

  3. 4. Mnapoanza sehemu kuu mpya ya kitabu, soma maelezo ya wazo kuu na utaje baadhi ya vichwa vinavyozungumziwa katika somo hilo.

  4. 5. Mnapomaliza sehemu kuu, tumia sehemu ya mambo makuu kumsaidia mwanafunzi wako akumbuke kweli alizojifunza.

  5. 6. Unapojifunza kila somo na mwanafunzi wako:

    1. Someni maelezo.

    2. Someni maandiko yote yaliyoandikwa “Soma.”

    3. Ikihitajika, someni maandiko mengine yaliyotajwa.

    4. Cheza video zote zilizoandikwa “Onyesha” (ikiwa zinapatikana).

    5. Muulize mwanafunzi kila swali lililo katika somo.

    6. Mwambie mwanafunzi wako atazame picha zilizo katika sehemu ya “Chimba Zaidi” kisha mwombe atoe maelezo kuhusu picha hizo.

    7. Tumia sanduku la “Lengo” kumsaidia mwanafunzi wako afuatilie maendeleo yake ya kiroho. Unaweza kumtia moyo atumie lengo lililotajwa, au ajiwekee malengo mengine, au afanye mambo yote mawili.

    8. Muulize mwanafunzi wako ikiwa alifurahia makala au video fulani hususa zilizo katika sehemu ya “Chunguza Zaidi” alipokuwa akitayarisha somo.

    9. Jitahidi kumaliza somo moja kila mnapojifunza.

Baada ya funzo

  1. 7. Endelea kumfikiria mwanafunzi wako. Mwombe Yehova abariki maendeleo ya mwanafunzi wako na akupatie hekima ili ujue jinsi ya kumsaidia.