Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Matangazo

Matangazo

KAZI YA KUJITOLEA Kama unapenda kujitolea juu ya kusaidia kufanya kazi ku mukusanyiko, tafazali ujulishe ndugu wenye kusimamia Biro ya Wafanyakazi Wenye Kujitolea.

MATUNZO YA KWANZA Tafazali, ukumbuke kama hii biro inatoa tu matunzo ya haraka.

MICHANGO Tumetumia makuta mingi juu tupate fasi ya muzuri ya kufanyia mukusanyiko wetu, vyombo vya muzuri vya sauti na video, na juu tufanye mambo ingine ili tufurahie mukusanyiko wetu na tumukaribie Yehova zaidi. Michango yenu ya kujipendea inasaidia kulipia ile mambo yote na kutegemeza kazi yenye kufanywa mu dunia yote. Visanduku vya michango vyenye kuonekana wazi vinapatikana nafasi mbalimbali mahali hapa. Munaweza pia kutoa michango kupitia Enternete ku donate.pr418.com. Michango yenu yote ni ya maana sana. Baraza Yenye Kuongoza inawashukuru kwa michango yenye munatoa kwa moyo wote juu ya kutegemeza faida za Ufalme.

UBATIZO Ikiwa hakuna mabadiliko yoyote, viti vya mbele ya jukwaa vitatayarishwa kwa ajili ya wale wenye watabatizwa. Wale wenye watabatizwa wanapaswa kuikala pale Siku ya Posho asubui mbele hotuba ya ubatizo ianze. Kila mumoja wao anapaswa kuwa na nguo ya kujipanguza nayo maji na manguo yenye kustahili ya kubatizwa nayo.

VITI Tafazali, ufikirie wengine. Kumbuka kama unaweza kuchunga tu viti kwa ajili ya watu wa familia yako, watu wenye umekuya nao mu gari moya, watu wenye unaikala nao mu nyumba moya, ao watu wenye unajifunza nao Biblia kwa sasa. Tafazali, usitie vitu ku viti vyenye hauchungiane.

VITU VYENYE VILILOKOTWA Kama unalokota kitu fulani na haujue mwenye nayo, tafazali uipeleke ku Biro ya Vitu Vyenye Vililokotwa. Kama umepoteza kitu fulani, uende ku ile biro juu uone kama kuko mwenye aliilokota. Mutoto mwenye amepotea, anapaswa kupelekwa ku ile biro. Lakini, ili kujiepusha na wasiwasi yenye inatokana na kupoteza mutoto, tafazali muchunge watoto wenu na muikale pamoya nao.

WAKARIBISHAJI Ndugu wenye kukaribisha watu wako tayari kukusaidia. Tafazali, uwasikilize na ufuate maagizo yao kuhusu fasi ya kuweka gari, fasi ya kuingilia na kutokea, ao maagizo kuhusu kuchungia wengine viti, na mambo ingine.

Ulitayarishwa na Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova

© 2024 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania