Ona video zinazopatikana

Kumujua Yehova Kutakuletea Faida

Kumujua Yehova Kutakuletea Faida

Kumujua Yehova Kutakuletea Faida

UNAWAZA kuko kitu fulani yenye inaweza kufanya maisha yako ikuwe muzuri? Watu wengi wameona kama kumujua Mungu kumefanya maisha yao ikuwe muzuri. Ukimujua Mungu utapata faida leo na mu siku zenye ziko nakuya.

Yehova Mungu, mwenye aliandikisha Biblia anapenda umujue. Muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: “Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” Ule muandikaji wa zaburi alitambua kama kujua Mungu kutatuletea faida. “Mimi, Yehova, niko Mungu wako, Mwenye anakufundisha ili ujipatie faida.” Tutapata faida gani kama tunamujua Yehova, Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi?​—Zaburi 83:18; Isaya 48:17.

Wakati tunamujua Mungu, tunapata mashauri yenye inasaidia kupiganisha magumu ya kila siku, tunakuwa na tumaini, na amani ya akili. Pia, wakati tunamujua Yehova muzuri zaidi, tunapata majibu ya maulizo ya maana sana yenye watu wengi wanajiulizaka mu maisha. Ni maulizo gani?

Maisha Iko na Kusudi?

Hata kama leo teknolojia inaendelea sana, haisaidie watu kupata majibu kwa hii maulizo: Juu ya nini niko hapa ku dunia? Maisha yangu ya kesho itakuwa namna gani? Maisha iko na kusudi gani?’ Kama mutu hapate majibu ya muzuri ku ile maulizo, hawezi kuwa na furaha ya kweli. Watu wengi wanawazaka kama maisha haina kusudi. Mu mwaka wa 1997, mu inchi ya Alemanye, watu wengi waliulizwa ikiwa maisha iko na kusudi. Nusu kati yao walijibia kama mara mingi ao wakati fulani, wanawazaka kama maisha haina kusudi. Pengine fasi kwenye unaishi watu wanawazaka pia vile.

Kama mutu anawaza maisha haina kusudi, anaweza kuona kama maisha ni bure na anaweza kushindwa kufanya mipango kwa ajili ya siku zenye ziko nakuya. Juu ya kujaribu kufanya maisha yao ikuwe na kusudi, watu wengi wanajikaza sana kutafuta kazi ya muzuri na kuwa matajiri. Hata vile, wanajisikia tu kama kuko kitu yenye wanakosa. Kukosa kusudi mu maisha kunafanyaka wengine wafikie hata kupoteza hamu ya kuishi. Mambo ya vile ilifikia mwanamuke mumoja kijana mwenye sura ya muzuri. Gazeti moja (International Herald Tribune) inasema kama alikomalia mu familia yenye kuwa na mali mingi. Hata kama aliishi maisha ya raha, alikuwa anajisikia kuwa peke yake na aliona kama maisha yake ilikuwa ya bure. Alikunywa dawa za mingi za usingizi na wakamukuta amekufa. Pengine na weye unajua watu fulani wenye walifikiaka kujiua juu ya kukosa furaha.

Watu fulani wanaamini kama sayansi inaweza kujibia maulizo yote yenye tunajiulizaka juu ya maisha. Gazeti moja ya Alemanye (Die Woche) inasema kama hata kama sayansi inaweza kufasiria mambo mingi, haiwezi kutusaidia tukuwe na urafiki pamoja na Mungu. Fundisho ya mageuzi (évolution) na mafundisho ingine ya sayansi yenye kuwa nguvu, haitupatie kitulizo na usalama. Sayansi imetusaidia kujua mambo mingi juu ya maisha. Lakini, haiwezi kutusaidia kujua sababu gani tunaishi na namna maisha yetu itakuwa wakati wenye kuja. Kama tunatumainia sayansi tu, hatutapata majibu ya maulizo yenye tunajiulizaka juu ya maisha. Gazeti moja inaonyesha kama ile inafanya mu dunia yote watu wakuwe na lazima sana ya mashauri ya kuwaongoza.

Muumbaji wetu tu njo anaweza kutupatia mashauri ya kutuongoza. Yeye njo anajua juu ya nini tuko hapa ku dunia, juu yeye njo alitutiaka hapa. Biblia inasema kama Yehova aliumba wanadamu juu wajaze dunia na kuitunza. Mu mambo yote yenye wanadamu wanafanya, Mungu alipenda waonyeshe sifa zake, sawa vile haki, hekima, na upendo. Kama tunaelewa juu ya nini Yehova alituumba, tutajua pia juu ya nini tuko hapa ku dunia.​—Mwanzo 1:26-​28.

Unaweza Kufanya Nini?

Utafanya nini kama ulishakakosa majibu ya muzuri ku hii maulizo: ‘Juu ya nini niko hapa ku dunia? Maisha yangu ya kesho itakuwa namna gani? Maisha iko na kusudi gani?’ Biblia inakutia moyo ujikaze kumujua Mungu muzuri. Yesu alisema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.” Biblia inakutia pia moyo uonyeshe sifa zenye Yehova anaonyeshaka, zaidi sana upendo, na uonyeshe kama unapenda kutawaliwa na Ufalme wa Mungu. Ukifanya vile, maisha yako itakuwa na kusudi, na utakuwa na tumaini ya muzuri. Pia, utapata majibu ya maulizo ya maana yenye ilikuwa inakuhangaisha.​—Yohana 17:3; Muhubiri 12:13.

Majibu ya ile maulizo inaweza kukusaidia namna gani? Tuone namna ilisaidia mwanaume mumoja mwenye kuitwa Hans. * Miaka fulani yenye imepita, Hans alikuwa anaamini kama Mungu anakuwaka. Lakini, hakukuwa anahangaikia mambo ya Mungu. Hans alikuwa anatumia dawa za kulewesha, alikuwa anafanya uasherati na wanamuke mbalimbali, alikuwa anafanya matendo ya kidogo-kidogo ya kuvunja sheria, na alikuwa anapenda kutembeza pikipiki. Lakini Hans anasema kama maisha yake haikukuwa na maana na hakukuwa na furaha. Wakati alikuwa na miaka karibu 25, Hans aliamua kujifunza juu ya Mungu kwa kusoma Biblia kwa uangalifu. Wakati Hans alifikia kumujua Yehova muzuri zaidi, na kuelewa kusudi ya maisha, alibadilisha maisha yake, akabatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Amekuwa mu utumishi wa wakati wote kwa miaka kumi yenye imepita. Anasema hivi: “Kumutumikia Yehova njo jambo ya maana sana mu maisha. Hakuna kitu yenye kuwa sawa na kumutumikia Yehova. Kumujua Yehova kumefanya maisha yangu ikuwe na kusudi.”

Zaidi ya kutafuta kujua kusudi ya maisha, kuko maulizo ingine yenye wanadamu wanajiulizaka. Kadiri hali ya ulimwengu inaendelea kuharibika, watu wako na lazima ya kupata jibu ya ulizo ingine ya maana.

Juu ya Nini Mambo ya Mubaya Inatokeaka?

Wakati watu wanateseka, wanajiulizaka hii ulizo: Juu ya nini mambo ya mubaya inatokeaka? Kama unaelewa juu ya nini mambo ya mubaya inatokeaka, itakuwa mwepesi zaidi kwako kuvumilia magumu na hautahuzunika kupita kiasi. Tuzungumuzie mufano wa mwanamuke fulani mwenye kuitwa Bruni.

Bruni anasema hivi: “Miaka fulani yenye imepita, mutoto wangu mwanamuke alikufa. Kwa sababu nilimuamini Mungu, nilienda kwa padri wa mu eneo yetu ili anifariji. Aliniambia kama Mungu njo alikuwa ameita Suzanne mbinguni, na kama sasa Suzanne amekuwa malaika. Nilihuzunika sana, na zaidi ya ile, nilimuchukia Mungu kwa sababu alikuwa amebeba mutoto wangu.” Bruni alihuzunika na kuteseka kwa miaka mingi. Anasema tena hivi: “Kisha, Mashahidi wa Yehova walinionyesha mu Biblia kama sikukuwa na sababu ya kumuchukia Mungu. Yehova hakumuita Suzanne aende mbinguni, na Suzanne hakukuwa sasa malaika. Kama aligonjwa, ni juu wanadamu hawakamilike. Susanne analala katika kifo. Na iko anangoya Yehova amufufue. Nilifikia pia kujua kama Yehova aliumba wandamu ili waishi milele mu paradiso ku dunia, na ni vile mambo itakuwa karibuni. Wakati nilianza kuelewa Yehova ni mutu wa namna gani kabisa, nilimukaribia zaidi, na huzuni yangu ilianza kupunguka.”​—Zaburi 37:29; Matendo 24:15; Waroma 5:12.

Watu wengi sana wako wanateseka mu njia mbalimbali. Kila mutu iko na magumu yake. Na kuko magumu ingine, sawa vile vita, njala, ao misiba ya asili. Bruni alipata kitulizo wakati aliona mu Biblia kama haiko makosa ya Yehova kama tuko tunateseka, kama Yehova hakupendaka wanadamu wakuwe wanateseka, na kama hivi karibuni atamaliza mambo yote ya mubaya. Kuona namna mambo ya mubaya iko inaendelea kuongezeka, kunaonyesha kama tuko tunaishi mu “siku za mwisho.” Siye wote tunapenda mambo ikuwe muzuri, na ni vile itakuwa karibuni.​—2 Timoteo 3:1-5; Matayo 24:7, 8.

Unaweza Kufanya Nini ili Umujue Mungu

Hans na Bruni hawakukuwa wanajua mambo mingi juu ya Mungu. Walikuwa wanamuamini, lakini hawakukuwa wanamujua muzuri. Wakati walijikaza kumujua Yehova muzuri zaidi, walipata faida mingi. Walipata majibu ya maulizo ya maana sana yenye walikuwa wanajiuliza. Ile iliwasaidia wakuwe na amani ya akili na wakuwe na tumaini. Watu mingi wenye kumutumikia Yehova wamepata ile faida.

Ili kumujua Yehova, unapaswa kwanza kujifunza Biblia. Biblia inatuambia mambo mingi juu yake na inatuambia mambo yenye anapenda tufanye. Ni vile watu fulani wenye waliishi wakati wa mitume walifanya. Luka aliandika kama Wakristo wa kutaniko ya Wayahudi yenye ilikuwa Beroya, Ugiriki, “walikubali neno kwa hamu kubwa ya akili [neno yenye Paulo na Sila waliwahubiria], na walikuwa wanachunguza Maandiko kila siku ili kuona kama mambo hayo yalikuwa vile.”​—Matendo 17:10, 11.

Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa pia wanakutana pamoja mu makutaniko. (Matendo 2:41, 42, 46; 1 Wakorinto 1:1, 2; Wagalatia 1:1, 2; 2 Watesalonike 1:1) Ni vile pia leo. Mashahidi wa Yehova wanakutanaka pamoja mu makutaniko mbalimbali. Mikutano yao iko na kusudi ya kusaidia kila mutu amukaribie Yehova, na afurahie kumutumikia. Mashahidi wa Yehova wanajikazaka sana kumuiga Yehova. Kama unazoea kuenda ku mikutano yao, ile itakusaidia na weye pia umuige Yehova na itakusaidia umujue muzuri zaidi.​—Waebrania 10:24, 25.

Kuko faida ya kujikaza sana vile juu tu ya kujua mutu mumoja? Njo vile, inaomba kujikaza. Ni vile mutu anafanyaka kama anapenda kupata jambo fulani ya maana mu maisha. Fikiria mambo yenye watu wanapaswa kufanya juu wapate ushindi mu michezo ya mukubwa-mukubwa ya kimataifa. Jean-Claude Killy, muchezaji mumoja mwenye alipataka ushindi ku michezo ya olimpike, alisema hivi: “Unapaswa kuanza kujitayarisha kwa ajili ya ile michezo miaka 10 mbele ianze. Na unapaswa kujizoeza na kuifikiria kila siku. . .” Mutu anatumia miaka mingi ya maisha yake juu tu ya kujitayarisha kwa ajili ya muchezo wenye pengine utafanya tu dakika 10! Kwa hiyo, ni jambo ya maana hata zaidi kujikaza kumujua Yehova kwa sababu kufanya vile kutatusaidia tupate faida za mingi sana, tena za milele.

Tutaendelea Kumukaribia Mungu

Siye wote tunapenda maisha yetu ikuwe na kusudi. Kwa hiyo, ikiwa unaona kama maisha yako haina kusudi, ao unapenda kujua juu ya nini mambo ya mubaya inatokeaka, ujikaze kumujua Yehova. Kujifunza juu yake kutafanya maisha yako ikuwe muzuri zaidi, milele.

Kuko siku tutaachaka kujifunza juu ya Yehova? Hata watu wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi wangali wanajifunza mambo ya mupya juu yake. Kama na siye tunafanya vile, tutakuwa na furaha na tutamukaribia hata zaidi. Kwa kweli, utakubaliana na maneno ya mutume Paulo mwenye aliandika hivi: “Oh! Utajiri wa Mungu na hekima na ujuzi ni kubwa sana! Hukumu zake haziwezi kuchunguzika na kutafutika kabisa! Kwa maana ‘ni nani amefikia kujua akili ya Yehova, ao ni nani amekuwa mushauri wake?’”​—Waroma 11:33, 34.

[Maelezo ya chini]

^ Majina fulani imebadilishwa.

[Wazo la fungu]

Watu wangali wanajiuliza hii maulizo ya maana: ‘Juu ya nini niko hapa ku dunia? Maisha yangu ya kesho itakuwa namna gani? Maisha iko na kusudi gani?’

[Wazo la fungu]

“Wakati nilianza kuelewa Yehova ni mutu wa namna gani kabisa, nilimukaribia zaidi”

[Wazo la fungu]

“Kumutumikia Yehova njo jambo ya maana sana mu maisha. Hakuna kitu yenye kuwa sawa na kumutumikia Yehova. Kumujua Yehova kumefanya maisha yangu ikuwe na kusudi”