Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Siku ya Kukumbuka

Siku ya Kukumbuka

Siku ya Kukumbuka

SIKU hiyo ilibadili kabisa wakati ujao wa wanadamu nao wangeweza kuwa na tumaini la kupata baraka za milele. Hakuna siku nyingine ambayo imeathiri wakati ujao wa wanadamu kama hiyo. Siku hiyo, Yesu alitimiza yote aliyokuja kufanya duniani. Akiwa amepigiliwa misumari kwenye mti wa mateso, Yesu alisema hivi kabla tu ya kufa: “Imetimizwa!” (Yohana 19:30) Kwa nini Yesu alikuja duniani?

Biblia inasema: ‘Mwana wa binadamu alikuja, si kuhudumiwa, bali kuhudumu na kutoa nafsi yake kuwa fidia katika kubadilishana kwa ajili ya wengi.’ (Mathayo 20:28) Yesu alitoa nafsi au uhai wake, ili wanadamu waweze kukombolewa kutoka katika dhambi na kifo walichorithi. Naam, “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akatoa Mwana mzaliwa-pekee wake, ili kila mtu anayedhihirisha imani katika yeye asipate kuangamizwa bali awe na uhai udumuo milele.” (Yohana 3:16) Dhabihu ya Yesu ina thamani kubwa kama nini!

Kuna sababu nyingine ya kukumbuka siku ambayo Yesu alikufa. Siku hiyo Mwana wa Mungu aliwafundisha mitume wake mambo muhimu sana ambayo yangewasaidia kuendelea kuwa waaminifu. Bila shaka, maneno yake ya mwisho yaligusa sana mioyo ya wanafunzi hao! Aliwafunza mambo gani? Tunaweza kunufaikaje na mambo ambayo Yesu aliwafunza? Maswali hayo yatazungumziwa katika makala inayofuata.