Ona video zinazopatikana

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Watu Wenye “Hawako Waamini” Wenye Paulo Anazungumuzia mu 2 Wakorinto 6:14, Ni Nani?

2 Wakorinto 6:14 inasema hivi: Musifungwe nira yenye haiko sawa pamoja na watu wenye hawako waamini.” Kama tunachunguza maandiko yenye kufuata tunaona kama Paulo alikuwa anazungumuzia watu wenye hawako mu kutaniko ya Kikristo. Ile inapatana na maandiko ingine yenye Paulo aliandika yenye kuwa na maneno “mwenye haiko mwamini” ao “wenye hawako waamini.”

Kwa mufano, Paulo alikaripia Wakristo juu walikuwa wanaenda ku tribinali “mbele ya wenye hawako waamini.” (1 Wakorinto 6:6) Mu ile andiko, wenye hawako waamini ni waamuzi wa tribinali ya Korinto. Mu barua yake ya pili, Paulo anasema kama Shetani “amepofusha akili za wenye hawaamini.” Mu ile andiko, macho ya wenye hawaamini ‘inafunikwa kitambaa’ juu isione habari njema. Wale watu wenye hawaamini hawayaonyesha kama wanapenda kumutumikia Yehova juu Paulo alisema hivi mu andiko yenye kutangulia: “Wakati mutu anageuka kumuelekea Yehova, kitambaa kinaondolewa.”​—2 Wakorinto 3:16; 4:4.

Watu fulani wenye hawako waamini wanafanyaka matendo ya kuvunja sheria ao kuabudu sanamu. (2 Wakorinto 6:15, 16) Lakini, haiko wote njo wanapingaka watumishi wa Yehova. Wengine wanapenda kujifunza kweli. Wengi wako na bibi ao Bwana Mukristo na wanafurahia kuendelea kuishi naye. (1 Wakorinto 7:12-14; 10:27; 14:22-25; 1 Petro 3:1, 2) Hata vile, wakati Paulo anatumia maneno “mwenye haiko mwamini,” sawa vile tulishasema, anamaanisha wale wenye hawako mu kutaniko ya Kikristo, yenye kufanyizwa na “wale wenye kumuamini Bwana.”​—Matendo 2:41; 5:14; 8:12, 13.

Kanuni yenye kuwa mu 2 Wakorinto 6:14 inaweza kusaidia Wakristo mu sehemu mbalimbali za maisha. Lakini inaweza kusaidia zaidi sana wale wenye wako natafuta mutu wa kuoana naye. (Matayo 19:4-6) Mukristo mwenye amejitoa kwa Yehova na kubatizwa, hapaswe kutafuta-tafuta mutu wa kuoana naye kati ya watu wenye hawako waamini juu kanuni zao, miradi yao, na mambo yenye wanaamini iko tofauti kabisa na ya Mukristo wa kweli.

Lakini, tuseme nini juu ya mutu mwenye anajifunzaka Biblia na anafikaka ku mikutano? Tuseme nini juu ya wahubiri wenye hawayabatizwa? Wao pia ni watu wenye hawako waamini? Hapana. Watu wenye wamekubali habari njema na wako nafanya maendeleo juu wafikie kubatizwa hawapaswe kuitwa watu wenye hawako waamini. (Waroma 10:10; 2 Wakorinto 4:13) Mbele Kornelio abatizwe, Biblia inasema kama alikuwa “muabudu wa Mungu na alikuwa anamuogopa Mungu.”​—Matendo 10:2.

Juu 2 Wakorinto 6:14 haihusu muhubiri mwenye hayabatizwa, ni jambo ya hekima kwa Mukristo mwenye kubatizwa kufanya uchumba na kuoana na muhubiri mwenye hayabatizwa? Hapana, haiko jambo ya hekima. Juu ya nini? Juu ya shauri yenye kuwa wazi yenye Paulo alipatia wajane Wakristo. Paulo aliandika hivi: “Iko huru kuolewa na mutu yeyote mwenye anataka, katika Bwana tu.” (1 Wakorinto 7:39) Ile shauri ya Paulo, inatia moyo Wakristo wenye kujitoa kwa Yehova watafute mutu wa kuoana naye kati ya wale wenye wako “katika Bwana tu.”

Maneno “katika Bwana” na maneno ingine yenye kufanana nayo, “katika Kristo,” maana yake nini? Mu Waroma 16:8-10 na mu Wakolosai 4:7 Paulo anazungumuzia watu wenye walikuwa katika Kristo ao katika Bwana. Kama unasoma ile maandiko utaona kama anawaita ‘wafanyakazi wenzake,’ ‘wenye kukubaliwa,’ ‘wapendwa wake,’ ‘watumishi waaminifu,’ na ‘watumwa wenzake.’

Ni wakati gani njo mutu anakuwaka “mutumwa katika Bwana”? Mutu anakuwa mutumwa katika Bwana wakati anafanya mambo yenye mutumwa anapaswa kufanya na wakati anajikana. Yesu alisema hivi: “Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, achukue muti wake wa mateso na aendelee kunifuata.” (Matayo 16:24) Mutu anaanza kumufuata Kristo wakati anafanya mapenzi ya Mungu na kujitoa kwa Mungu. Kisha pale, anabatizwa na kuwa mutumishi mwenye kukubaliwa na Yehova Mungu. * Kwa hiyo, ‘kuoa ao kuolewa katika Bwana’ maana yake kuoa ao kuolewa na mutu mwenye ameonyesha kabisa kama iko muamini, ni kusema iko “mutumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo.”​—Yakobo 1:1.

Mutu mwenye iko najifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova na iko nafanya maendeleo, iko nafanya muzuri. Lakini, hayajitoa kwa Yehova na kumuahidi kama atamutumikia maisha yake yote. Angali nafanya mabadiliko yenye inaomba kufanya mu maisha yake. Anapaswa kumaliza kufanya mabadiliko makubwa mu maisha yake na kujitoa kwa Mungu na kubatizwa mbele afikirie kufanya jambo ingine yenye itabadilisha sana maisha yake, sawa vile ndoa.

Ni jambo ya hekima kwa Mukristo kuanzisha uchumba na mutu mwenye funzo yake ya Biblia iko naendelea muzuri, pengine na mawazo ya kuchunga abatizwe juu waoane? Hapana. Ile inaweza kufanya mwanafunzi wa Biblia asifanye maendeleo na nia ya muzuri, juu anajua kama kuko Mukristo mwenye iko namungoya abatizwe kusudi waoane.

Mara mingi, mutu anakuwaka muhubiri mwenye hayabatizwa kwa wakati kidogo tu, mbele afanye maendeleo na kufikia kubatizwa. Njo maana, shauri ya kuoa ao kuolewa katika Bwana tu, yenye tulishazungumuzia, haitufunge. Lakini, tuseme nini kama mutu alishaeneza miaka ya kuoa ao kuolewa, alikomalia mu familia ya Kikristo, amekuwa mu kutaniko kwa miaka mingi, na ni muhubiri mwenye hayabatizwa? Kama ni vile, nini njo inamuzuia asitoe maisha yake kwa Yehova? Juu ya nini iko anasita-sita? Iko na mashaka? Ni kweli kama haiko mutu mwenye haamini, lakini pia hatuwezi kusema kama iko “katika Bwana.”

Mashauri yenye Paulo alitoa juu ya ndoa ni kwa faida yetu. (Isaya 48:17) Kama watu wawili wanapenda kuoana, wanapaswa kuwa wamejitoa kwa Yehova. Ile itawasaidia wakuwe na ndoa yenye kuwa na furaha juu wako na uhusiano muzuri pamoya na Yehova. Wanafuata kanuni zilezile na wako na miradi ileile. Ile inafanya ndoa yao ikuwe na furaha kabisa. Zaidi ya yote, wakati mutu ‘anaoa ao kuolewa katika Bwana tu,’ anaonyesha kama iko mushikamanifu kwa Yehova, na ile inafanya Yehova amubariki juu ‘kwa mutu mushikamanifu [Yehova] anatenda kwa ushikamanifu.’​—Zaburi 18:25.

[Maelezo ya chini]

^ Mutume Paulo alikuwa anaandikia kwanza Wakristo watiwa-mafuta. Kwa Wakristo watiwa-mafuta, kuwa “mutumwa katika Bwana” ilimaanisha pia kutiwa mafuta ili wakuwe wana wa Mungu na ndugu za Kristo.

[Picha]

‘Kwa mutu mushikamanifu [Yehova] anatenda kwa ushikamanifu’