Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Miujiza ya Yesu Inaweza Kukufundisha Nini?

Miujiza ya Yesu Inaweza Kukufundisha Nini?

Miujiza ya Yesu Inaweza Kukufundisha Nini?

Pengine utashangala kujua kama wakati Biblia inazungumuzia maisha ya Yesu ku dunia, haitumie neno ya kigiriki yenye inatafsiriwa “muujiza” (dyʹna·mis). Wakati fulani, neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa muujiza, inamaanisha “nguvu.” (Luka 8:46) Inaweza pia kutafsiriwa “uwezo” ao “kazi zenye nguvu.” (Matayo 11:20; 25:15) Mutu fulani mwenye elimu alionyesha kama ile neno ya Kigiriki “inakazia kazi zenye nguvu zenye mutu amefanya, na zaidi sana, nguvu yenye mutu alitumia juu ya kufanya zile kazi. Inaonyesha mambo yenye nguvu ya Mungu inatimiza.”

Neno ingine ya Kigiriki (teʹras) kwa kawaida inatafsiriwaka “jambo ya ajabu.” (Yohana 4:48; Matendo 2:19) Ile neno inaonyesha mawazo ya watazamaji juu ya jambo fulani. Mara mingi, watu na wanafunzi wa Yesu walikuwa wanashangala wakati walikuwa wanaona kazi zenye nguvu za Yesu.​—Marko 2:12; 4:41; 6:51; Luka 9:43.

Neno ya tatu ya Kigiriki yenye inatumiwa ili kuzungumuzia miujiza ya Yesu (se·meiʹon) inamaanisha “alama.” Robert Deffinbaugh anasema kama ile neno “inakazia maana ya ndani kabisa ya muujiza.” Anaongezea hivi: “Alama ni muujiza wenye unatufundisha jambo fulani juu ya Bwana Yesu.”

Miujiza Ilitoka Kabisa kwa Mungu Biblia haionyeshe kama miujiza ya Yesu ilikuwa tu mambo ya uchawi ya kufurahisha watu. Lakini Yesu alifanya ile miujiza kwa kutumia “nguvu kubwa za Mungu.” Kwa mufano alifukuza pepo muchafu ndani ya kijana fulani mwanaume. (Luka 9:37-​43) Biblia inasema kama Mungu iko na ‘nguvu nyingi zenye musukumo.’ Mungu Mweza-Yote anaweza kukosa nguvu ya kufanya ile miujiza ya ajabu? (Isaya 40:26) Hapana!

Vitabu vya injili vinazungumuzia miujiza 35 hivi yenye Yesu alifanya. Lakini havionyeshe miujiza yote yenye alifanyaka. Kwa mufano, Matayo 14:14 inasema hivi: “Wakati alifika pembeni ya bahari, akaona watu wengi sana, na akawasikilia huruma, na akaponyesha wagonjwa wao.” Biblia haiseme ni watu ngapi njo aliponyeshaka ile siku.

Miujiza yenye Yesu alifanya ilionyesha wazi kama alikuwa Mwana wa Mungu, na Masiya mwenye aliahidiwa. Maandiko inaonyesha kama nguvu yenye Yesu alitumikisha juu ya kufanya miujiza, ilitoka kwa Mungu. Mutume Petro alisema kama Yesu alikuwa “mwanaume mwenye Mungu alionyesha kwenu waziwazi kupitia matendo yenye nguvu na maajabu na alama zenye Mungu alifanya kupitia yeye katikati yenu, kama vile ninyi wenyewe munajua.” (Matendo 2:22) Wakati ingine, Petro alisemaka kama “Mungu alimutia mafuta kwa roho takatifu na nguvu, na akapita katika inchi akitenda mema na kuponyesha wote wenye walikandamizwa na Ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.”​—Matendo 10:37, 38.

Kazi ya Yesu ilitia ndani miujiza yake na mafundisho yake. Marko 1:21-​27 inaonyesha namna watu walijisikia wakati walisikia mafundisho ya Yesu, na kuona muujiza fulani wenye alifanya. Marko 1:22 inasema kama watu “walishangazwa na namna yake ya kufundisha,” na mustari wa 27 inaongeza kama watu “walishangaa sana” wakati alifukuza pepo muchafu. Miujiza ya Yesu na mafundisho yake ilionyesha kama alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa.

Yesu hakusema tu kama alikuwa Masiya; maneno yake na mambo yenye alifanya, kupitia nguvu yenye Mungu alimupatia, ilionyesha kama alikuwa Masiya. Wakati watu walimuuliza maulizo juu ya mamlaka yake na kazi yake, aliwajibia hivi bila woga: “Niko na ushahidi mukubwa kuliko ule wa Yohana, kwa maana kazi zenye Baba yangu alinipatia nitimize, ni kusema, kazi hizi zenye ninafanya, zinatoa ushahidi kwamba Baba alinituma.”​—Yohana 5:36.

Mambo Yenye Inaonyesha Kama Miujiza ya Yesu Ilifanyikaka Kabisa

Nini njo inaonyesha kama miujiza ya Yesu ilifanyikaka kabisa? Tuone mambo fulani yenye inaonyesha vile.

Wakati Yesu alikuwa anafanya miujiza, hakukuwa anapenda kujionyesha. Alikuwa anapenda heshima na utukufu vimuendee Mungu. Kwa mufano, mbele aponyeshe kipofu fulani, alisema kama ule kipofu ataponyeshwa “kusudi kazi za Mungu zifikie kufunuliwa kupitia yeye.”​—Yohana 9:1-3; 11:1-4.

Wachawi, wafumu, na waponyaji, wanafanyaka watu wapoteze ufahamu, wanatumiaka udanganyifu, wanafanyaka mambo ya kujionyesha, wanatupiaka watu ulozi, na kufanya desturi za ajabu-ajabu. Lakini Yesu yeye hakukuwaka vile. Hakukuwa anatumia ushirikina ao hirizi ili kuponyesha watu. Ona namna aliponyesha wanaume wawili vipofu, bila kufanya mambo ya ajabu-ajabu. Biblia inasema hivi: “Akawasikilia huruma, kwa hiyo akagusa macho yao, na mara moja wakaanza kuona tena, na wakamufuata.” (Matayo 20:29-​34) Hakufanya desturi za ajabu-ajabu, ao kutafuta kujionyesha wakati alikuwa nafanya miujiza. Yesu alikuwa nafanya miujiza yake ku macho ya watu wengi, hakutumia mwangaza fulani wa pekee, jukwaa ao vitu vingine vya ajabu-ajabu. Ile ni tofauti na watu wa leo wenye wanasema kama wanaweza kufanya miujiza, lakini hakuna jambo yenye kuhakikisha kama wanaweza kufanya vile.​—Marko 5:24-​29; Luka 7:11-​15.

Wakati fulani Yesu alikuwa naona kama wale wenye aliponyesha walikuwa na imani. Lakini Yesu hakukuwa anakatala kuponyesha mutu juu tu hana imani. Wakati alikuwa Kapernaumu katika Galilaya, “watu walimuletea watu wengi wenye walikuwa na pepo wachafu; akafukuza hao roho kwa kusema neno moja, na akaponyesha wote wenye walikuwa wagonjwa.”​—Matayo 8:16.

Yesu alifanya miujiza juu ya kusaidia watu, haiko juu ya kutafuta kuwashangaza. (Marko 10:46-​52; Luka 23:8) Na hakuna siku alifanyaka muujiza juu ya kujitafutia faida.​—Matayo 4:2-4; 10:8.

Vitabu vya Injili Vinasemaka Kweli?

Vitabu ine vya Injili njo vinatuelezea miujiza yenye Yesu alifanyaka. Tunaweza kuamini mambo yenye vile vitabu vinasema juu ya miujiza ya Yesu? Ndiyo.

Sawa vile tulishaona, Yesu alifanyaka miujiza yake mbele ya watu wengi. Vitabu vya kwanza vya Injili viliandikwa wakati watu wengi wenye walionaka miujiza ya Yesu walikuwa wangali wazima. Kitabu The Miracles and the Resurrection kinaonyesha kama waandikaji wa Injili waliandika mambo ya kweli. Kinasema hivi: “Ni kukosa haki kusema kama wenye waliandika vitabu vya Injili walisema uongo juu ya miujiza ya Yesu juu tu walipenda watu waamini mawazo yao. . . . Mambo yenye waliandika ni ya kweli.”

Wayahudi wenye walikuwa wanapinga Ukristo hawakusema kama miujiza yenye kuandikwa mu vitabu vya Injili haikufanyikaka. Walisema njo kama pepo wachafu njo walikuwa nasaidia Yesu kufanya miujiza. (Marko 3:22-​26) Hata kisha pale, wengine wenye walipinga Ukristo walishindwa kuonyesha kama miujiza ya Yesu haikufanyikaka. Mu karne ya kwanza na ya pili, kulikuwa hata maandishi yenye ilizungumuzia miujiza ya Yesu. Kwa kweli, tuko na sababu zenye kutuhakikishia kama mambo yenye vitabu vya Injili vinasema juu ya miujiza ya Yesu ni ya kweli.

Yesu Alikuwa Mutu wa Namna Gani?

Juu tuelewe kabisa miujiza yenye vitabu vya Injili vinazungumuzia, tunapaswa pia kujua muzuri mwenye alifanyaka ile miujiza. Vitabu vya injili vinatuambia kama Yesu alikuwa napenda sana watu, alikuwa na huruma na alihangaikia sana wengine.

Kwa mufano, mutu fulani mwenye ukoma alikuja kwa Yesu na kumulilia amusaidie. Alisema hivi: “Kama tu unataka, unaweza kunifanya nikuwe safi.” Yesu “akasikia huruma,” akanyoosha mukono, akamugusa na kumuambia hivi: “Ninataka! Kuwa safi.” Ule mwanaume akapona palepale. (Marko 1:40-​42) Ile inaonyesha kama Yesu alifanya miujiza juu alipenda watu na aliwahangaikia.

Yesu alifanya nini wakati alikutana na watu wenye walikuwa natoka mu muji wa Naini ile kuenda kuzika kijana fulani mwanaume? Ule kijana mwanaume alikuwa mutoto mumoja tu wa mujane fulani. “Yesu alisikilia huruma” ule mujane, akaenda karibu naye na kumuambia hivi: “Acha kulia.” Kisha akafufua mutoto wake.​—Luka 7:11-​15.

Miujiza ya Yesu inatufundisha jambo fulani ya kufurahisha sana: Alikuwa “anasikilia watu huruma” na alikuwa tayari kuwasaidia. Tena, miujiza ya Yesu inatupatia tumaini. Waebrania 13:8 inasema hivi: “Yesu Kristo ni uleule jana, leo, na milele.” Leo, Yesu iko Mufalme mbinguni, na iko tayari kufanya miujiza ya mingi sana kushinda hata miujiza yenye alifanyaka wakati alikuwaka ku dunia. Karibuni, Yesu atatumia nguvu yenye Mungu amemupatia juu ya kuponyesha wanadamu wote wenye kumutii Mungu. Mashahidi wa Yehova watafurahi sana kukusaidia kujifunza juu ya mambo ya muzuri sana yenye Mungu atafanya mu siku zenye ziko nakuya.

[Picha]

Yesu alifanya ile miujiza kwa kutumia “nguvu kubwa za Mungu.”

[Picha]

Yesu alikuwa nasikilia watu huruma