Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ujiwekee Miradi ya Kiroho Juu ya Kutukuza Muumbaji Wako

Ujiwekee Miradi ya Kiroho Juu ya Kutukuza Muumbaji Wako

Ujiwekee Miradi ya Kiroho Juu ya Kutukuza Muumbaji Wako

“KAMA mutu mwenye kuendesha mashua hajue kwenye iko naenda, upepo utamubeba fasi ni fasi.” Ile maneno yenye inaonekana ilisemwa na filozofe fulani Muroma wa karne ya kwanza, inaonyesha kama juu maisha yetu ikuwe na kusudi, inaomba tukuwe na miradi mu maisha.

Mu Biblia muko mifano ya watu wenye walijua kama ni jambo ya maana kujiwekea miradi. Kwa mufano, Noa alitumika miaka 50 ili ‘kujenga safina ili kuokoa nyumba yake.’ Nabii Musa “alikaza macho kwenye malipo ya zawabu.” (Waebrania 11:7, 26) Yoshua mwenye alikamata nafasi ya Musa, alikuwa na muradi wa kukamata inchi ya Kanaani; Mungu njo alimupatia ule muradi.​—Kumbukumbu la Torati 3:21, 22, 28; Yoshua 12:7-​24.

Wakati wa mitume, miradi yenye mutume Paulo alijiwekea ilichochewa na hii maneno ya Yesu: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Matayo 24:14) Paulo alisaidia sana kuanzisha makutaniko mu Asia Ndogo na mu Ulaya. Mambo yenye ilimuchochea kufanya vile ni ujumbe wa maono yenye alipokea kutoka kwa Yesu, na pia mugao wenye alipewa wa “kupeleka jina [la Yesu] kwa mataifa.”​—Matendo 9:15; Wakolosai 1:23.

Kwa kweli, tangu zamani watumishi wa Yehova wamejitilia miradi ya muzuri na wameifikia ili kumutukuza Mungu. Namna gani tunaweza kujiwekea miradi ya kiroho leo? Tunaweza kujiwekea miradi gani, na tunaweza kufanya nini juu tuifikie?

Inaomba Kuwa na Nia ya Muzuri

Tunaweza kujitilia miradi mu mambo mbalimbali. Mu dunia muko pia watu wenye wanafanyaka vile. Lakini miradi ya kiroho iko tofauti na miradi yenye watu wanajiwekeaka mu hii dunia juu ya kutafuta makubwa. Wakati watu wengi wanajitilia miradi mu hii dunia, nia yao kubwa inakuwaka kupata makuta, kuwa na cheo, ao mamlaka. Ni kukosa kabisa hekima kujitilia muradi fulani juu tu ya kutafuta cheo na kutafuta kujulikana! Tunamutukuza Yehova Mungu wakati tunajiwekea miradi yenye inatusaidia tumutumikie na tutegemeze kazi ya Ufalme. (Matayo 6:33) Tunajitilia ile miradi juu tunapenda Mungu na wanadamu wenzetu na juu tunapenda kushikamana na Mungu.​—Matayo 22:37-​39; 1 Timoteo 4:7.

Tunapaswa kuwa na nia ya muzuri wakati tunajitilia miradi ya kiroho na kujikaza kuifikia, ikuwe muradi wetu ni kufikia mapendeleo fulani mu tengenezo ya Yehova ao kukomalisha sifa fulani za kiroho. Lakini, hata tukuwe na nia ya muzuri, kuko miradi fulani yenye tunaweza kushindwa kufikia. Nini njo inaweza kutusaidia kufikia miradi yetu?

Tunapaswa Kuwa na Tamaa Kubwa ya Kufikia Miradi Yetu

Fikiria namna Yehova alitimiza kazi yake ya kuumba ulimwengu. Maneno “ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui,” inaonyesha kama Yehova alipanga kazi yake mu vipindi mbalimbali. (Mwanzo 1:5, 8, 13, 19, 23, 31) Ku mwanzo wa kila kipindi ya uumbaji, alikuwa anajua muradi wake ni nini, ni kusema alikuwa anajua mambo yenye atafanya ile siku. Kwa kufanya vile, alitimiza kusudi yake ya kuumba vitu. (Ufunuo 4:11) Yobu alisema hivi: “Wakati [Yehova] anataka kufanya jambo fulani, yeye analifanya.” (Yobu 23:13) Kwa kweli Yehova alifurahi sana wakati aliona “kila kitu chenye alikuwa amefanya,” na akasema ni “kizuri sana”!​—Mwanzo 1:31.

Juu na siye tufikie miradi yetu tunapaswa kuwa na nia kabisa ya kuifikia. Nini njo itatusaidia tukomalishe ile tamaa ya kufikia miradi yetu? Hata wakati dunia ilikuwa bila umbo na bila kitu, Yehova alikuwa alishaona namna itafikia kuwa fasi ya kupendeza sana, yenye itamuletea utukufu. Vilevile, kama tunafikiria matokeo ya muzuri na faida yenye tutapata kama tunafikia miradi yetu, tutakuwa na tamaa kubwa ya kuifikia. Ni vile Tony mwenye kuwa na miaka 19 alifanya. Hakusahau hata kidogo namna alijisikiaka wakati alitembeleaka biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Ulaya ya Mangaribi. Kuanzia ile siku, ulizo yenye ilikuwa narudia mu akili yake ni hii: ‘Maisha itakuwa namna gani kama ninaishi na kutumikia fasi ya vile?’ Tony aliendelea kufikiria ile jambo, na alijikaza sana juu afikie muradi wake. Kisha miaka fulani alifurahi sana wakati ombi yake ya kutumikia ku biro ya tawi ilikubaliwa!

Kama tunafanya urafiki na watu wenye walishafikia miradi yao, ile inaweza kutuchochea na siye tukuwe na tamaa ya kufikia miradi yetu. Tufikirie mufano wa Jayson, mwenye kuwa na miaka 30. Wakati alikuwa kijana, hakukuwa anafurahia mahubiri. Lakini kisha kumaliza masomo ya segondere, akakuwa painia, na kwa hiyo akakuwa mutumishi wa wakati wote. Nini njo ilisaidia Jayson akuwe na tamaa ya kuwa painia? Anajibia hivi: “Kuzungumuza na mapainia wengine na kuhubiri pamoya nao njo kulinisaidia sana.”

Tuandike Miradi Yetu

Wakati tunaeleza mawazo yetu, inakuwa mwepesi kuielewa. Sulemani alisema kama maneno yenye kufaa inaweza kuwa yenye nguvu kama vile michokoo ya ngombe, ni kusema inaweza kutuongoza mu maisha. (Muhubiri 12:11) Wakati tunaandika ile maneno, inabakia kabisa mu akili yetu na mu moyo wetu. Njo maana Yehova aliambia wafalme wa Israeli wajiandikie kopi ya Sheria. (Kumbukumbu la Torati 17:18) Kwa hiyo, ni muzuri tuandike miradi yetu, mambo yenye tutafanya juu ya kuifikia, vizuizi vyenye tunaweza kupata, na namna ya kushinda vile vizuizi. Ni muzuri pia kujua habari zenye tunapaswa kujifunza, ufundi wenye tunapaswa kuwa nao, na watu wenye wanaweza kutusaidia na kututegemeza.

Geoffrey, alikuwa painia wa pekee kwa muda murefu mu inchi fulani ya Asia. Kujitilia miradi kulimusaidia atulie na akuwe na amani ya akili. Alipata magumu wakati bibi yake alikufa kwa kushitukia. Iliomba wakati juu azoee hali yake ya mupya. Kisha aliamua kujitilia miradi yenye ilimusaidia akuwe na mambo mingi ya kufanya mu kazi yake ya upainia. Kisha kuandika miradi yake, alimuomba Yehova amusaidie juu aanzishe mafunzo tatu ya Biblia kufikia mwisho wa mwezi. Kila siku alikuwa anachunguza kazi yake ya kuhubiri, na kisha kila siku kumi alikuwa anachunguza maendeleo yenye amefanya. Alifikia muradi wake? Ndiyo, juu alianzisha mafunzo ine ya Biblia!

Ujiwekee Kwanza Miradi ya Kidogo-kidogo

Ku mwanzo, miradi fulani inaweza kuonekana kuwa nguvu kufikia. Tony, mwenye tulishazungumuzia, aliona kama muradi wa kutumikia ku biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ulikuwa sawa vile ndoto. Aliona vile juu alikuwa na mwenendo mubaya na alikuwa hayajitoa kwa Mungu na kubatizwa. Lakini Tony aliamua kutumikisha kanuni za Yehova mu maisha yake na kutimiza mambo yenye inaombwa juu astahili kubatizwa. Kisha kubatizwa, akakuwa painia musaidizi, na kisha akakuwa painia wa kawaida. Alikuwa ameandika ku karatasi tarehe yenye atakuwa painia musaidizi na tarehe yenye atakuwa painia wa kawaida. Kisha kuwa painia kwa wakati fulani hakuona tena kama muradi wa kutumikia ku biro ya tawi ni ndoto.

Ni muzuri na siye tujitilie miradi ya kidogo-kidogo yenye itatusaidia kufikia miradi kubwa-kubwa. Tunapaswa pia kuchunguza kwa ukawaida maendeleo yetu, ile itasaidia kuona nini njo inabakia juu tufikie miradi yetu. Kuambia Yehova mara kwa mara miradi yetu, kutatusaidia tuendelee kujikaza juu tuifikie. Mutume Paulo alitushauria hivi: “Musali bila kuacha.”​—1 Watesalonike 5:17.

Usichoke

Kuko miradi yenye tunaweza kushindwa kufikia hata kama tuko na mipango ya muzuri na tunatamani sana kuifikia. Kwa mufano, bila shaka mwanafunzi Yohana Marko alihuzunika sana wakati mutume Paulo alikatala kuenda naye mu safari yake ya pili ya umisionere! (Matendo 15:37-​40) Ile mambo yenye ilifikia Marko ilimufundisha somo fulani na akabadilisha miradi yake juu afanye mambo mingi zaidi mu kazi ya Yehova. Kisha wakati fulani Paulo alisema mambo ya muzuri juu ya Marko, na Marko alitumika sana na mutume Petro mu muji wa Babiloni. (2 Timoteo 4:11; 1 Petro 5:13) Pengine pendeleo kubwa zaidi yenye alipata ilikuwa kuandika habari juu ya maisha na utumishi wa Yesu.

Kuko mambo yenye inaweza kutuzuia na siye tusifikie miradi yetu. Wakati tunajikuta mu ile hali, tusivunjike moyo. Tuchunguze tena miradi yetu, na tubadilishe miradi yetu kama ni lazima. Wakati tunapata vizuizi, tusichoke, tuendelee kujikaza juu tufikie miradi yetu. Mufalme Sulemani anatuhakikishia hivi: “Tia kila jambo lenye unafanya katika mukono wa Yehova, na mipango yako itafanikiwa.”​—Mezali 16:3.

Lakini, hali zinaweza kufanya isiwezekane kufikia miradi fulani. Kwa mufano, afya ya mubaya ao madaraka ya familia inaweza kutuzuia tusifikie miradi fulani. Tusisahau hata kidogo kama zawadi yenye siye wote tutapata ku mwisho ni uzima wa milele, mbinguni ao ku dunia Paradiso. (Luka 23:43; Wafilipi 3:13, 14) Tunapaswa kufanya nini juu tupate ile zawadi? Mutume Yohana aliandika hivi: “Ule mwenye anafanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:17) Hata kama hali yetu haituruhusu kufikia muradi fulani, tunapaswa kuendelea ‘kuogopa Mungu wa kweli na kushika amri zake.’ (Muhubiri 12:13) Miradi ya kiroho inatusaidia kukaza akili juu ya kazi ya Yehova. Tujitilie basi miradi ya kiroho juu ya kumutukuza Muumbaji wetu.

[Kisanduku]

Miradi ya Kiroho Yenye Unaweza Kujitilia

○ Kusoma Biblia kila siku

○ Kusoma kila gazeti Munara wa Mulinzi na Amuka!

○ Kufanya sala zako zikuwe muzuri zaidi

○ Kuonyesha sifa za tunda la roho

○ Kufanya mambo mingi zaidi mu kazi ya Yehova

○ Kuwa mwenye ufundi zaidi mu kazi ya kuhubiri na kufundisha

○ Kukomalisha ufundi wa kuhubiri ku telefone, kuhubiri wakati wowote, na kuhubiri nafasi za biashara