Ona video zinazopatikana

“Kila Mutu Atabeba Muzigo Wake Mwenyewe”

“Kila Mutu Atabeba Muzigo Wake Mwenyewe”

“Kila Mutu Atabeba Muzigo Wake Mwenyewe”

“Kila mumoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.”​—WAROMA 14:12.

1. Waebrania watatu walipaswa kukamata uamuzi gani?

 WAEBRANIA watatu katika Babiloni wanapaswa kukamata uamuzi muzito sana. Watainamia sanamu kubwa sawa vile sheria ya inchi inaomba, ao watakatala kuiabudu na kisha watupwe mu tanuru yenye kuwaka moto? Shadraki, Meshaki, na Abednego hawana wakati wa kuomba mashauri kwa mutu mwingine; na hawaone kama ni lazima kufanya vile. Bila kusita, wanasema hivi: “Ujue, Ee mufalme, kama hatutatumikia miungu yako wala kuabudu sanamu ya zahabu yenye ulisimamisha.” (Danieli 3:1-18) Wale Waebrania watatu walibeba muzigo wao wenyewe.

2. Nani njo alichochea uamuzi wenye Pilato alikamata kuhusu Yesu, na ile ilifanya mambo yenye ilifikia Yesu isikuwe ku kichwa ya Pilato?

2 Miaka mia sita kisha pale, gavana fulani anasikiliza namna watu wako wanashitaki mwanaume fulani. Kisha kuchunguza ile mashitaka, anaona kama ule mwanaume hana kosa. Lakini watu wenye kuwa pale, wanasema kama ule mwanaume anapaswa kuuawa. Ku mwanzo, ule gavana anajaribu kutetea ule mwanaume. Lakini ku mwisho anafuata mambo yenye watu wako wanaomba na kwa kufanya vile, anashindwa kubeba muzigo wake. Ananawa mikono yake na kusema: “Sina kosa juu ya damu ya mutu huyu.” Kisha anaruhusu ule mwanaume atundikwe ku muti. Kuliko kuwa na uhodari wa kukamata uamuzi wake mwenyewe kuhusu Yesu Kristo, Pontio Pilato anaacha wengine waamue pa nafasi yake. Hata kama alinawa mikono, mambo yenye ilifikia Yesu, ilikuwa ku kichwa yake.​—Matayo 27:11-26; Luka 23:13-25.

3. Juu ya nini hatupaswe kuacha wengine watukamatie maamuzi?

3 Halafu weye? Wakati inaomba ukamate maamuzi, unafanyaka sawa vile wale Waebrania watatu, ao unaachaka wengine wakamate maamuzi pa nafasi yako? Haiko mwepesi kukamata maamuzi. Mutu anapaswa kukomala kiroho juu aweze kukamata maamuzi ya muzuri. Kwa mufano, wazazi wanapaswa kukamata maamuzi ya muzuri kwa ajili ya watoto wao wadogo. Kusema kweli, ni nguvu kukamata maamuzi wakati uko mu hali ya nguvu, na wakati kuko mambo ya mingi yenye inaomba ufikirie. Lakini, kukamata maamuzi haiko jambo nzito sana, mupaka tufikie kusema kama tunaweza kuitia kati ya “mizigo mizito,” yenye wale wenye kuwa na “sifa za kustahili kiroho” wanaweza kutubebea. (Wagalatia 6:1, 2) Lakini, ni muzigo wenye ‘kila mumoja wetu atatolea hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.’ (Waroma 14:12) “Kila mutu atabeba muzigo wake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) Sasa, tunaweza kufanya nini juu tukamate maamuzi ya muzuri mu maisha? Kwanza, tunapaswa kutambua kama siye wanadamu tuko na mipaka na pia tunapaswa kujua mambo yenye inaweza kutusaidia juu tukamate maamuzi ya muzuri.

Jambo ya maana sana yenye tunapaswa kufanya

4. Makosa ya Adamu na Eva inatufundisha nini kuhusu kukamata maamuzi?

4 Muda mufupi kisha Mungu kuumba Adamu na Eva, walikamata uamuzi wenye ulileta magumu mingi. Waliamua kula matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya. (Mwanzo 2:16, 17) Juu ya nini waliamua vile? Biblia inasema hivi: “Basi mwanamuke akaona kwamba muti huo ulikuwa wenye kufaa kwa chakula na ulikuwa kitu chenye kupendeza macho, ndiyo, muti huo ulikuwa wenye kupendeza macho. Kwa hiyo mwanamuke akaanza kukamata matunda ya muti huo na kuyakula. Kisha, wakati alikuwa pamoja na bwana yake, akamupatia pia, naye akaanza kuyakula.” (Mwanzo 3:6) Eva aliamua vile juu alikuwa najifikiria tu. Mambo yenye Eva alifanya ilichochea Adamu naye akule ile tunda. Matokeo ilikuwa nini? Zambi na kifo ‘vilienea kwa watu wote.’ (Waroma 5:12) Makosa ya Adamu na Eva inatufundisha hii jambo ya maana sana kuhusu mipaka yenye tuko nayo: Kama hatufuate muongozo wa Mungu, ni mwepesi tukamate maamuzi ya mubaya.

5. Yehova ametutolea muongozo gani, na tunapaswa kufanya nini juu itusaidie?

5 Tuko na furaha sana juu Yehova ametupatia muongozo! Biblia inatuambia hivi: “Masikio yako yatasikia neno nyuma yako likisema, “Hii ndiyo njia. Mutembee ndani yake,” ikuwe mutaenda upande wa kuume ao mutaenda upande wa kushoto.” (Isaya 30:21) Yehova anazungumuza na siye kupitia Neno yake Biblia yenye iliongozwa na roho yake. Tunapaswa kujifunza maandiko na kuijua muzuri. Juu tukamate maamuzi ya muzuri, tuko na lazima ya “chakula kigumu [chenye] ni cha watu wakomavu.” ‘Kwa kukitumia nguvu zetu za utambuzi zinazoezwa kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.’ (Waebrania 5:14) Tunazoeza nguvu zetu za utambuzi wakati tunatumia mambo yenye tunajifunza mu Biblia.

6. Zamiri yetu iko na lazima ya nini juu itumike muzuri?

6 Zamiri yetu inaweza pia kutusaidia kukamata maamuzi. Inaweza kutusaidia kuona ikiwa jambo fulani ni ya muzuri ao ni ya mubaya, na inaweza ‘kutushitaki ao hata kututetea.’ (Waroma 2:14, 15) Lakini juu zamiri yetu itumike muzuri, inapaswa kuongozwa na Neno ya Mungu na tunapaswa kutumikisha mambo yenye tunajifunza. Kama zamiri yetu haizoezwe muzuri, inaweza kuwa mwepesi kukamata maamuzi ya mubaya kwa kufuata desturi za kwetu ao mambo yenye watu wengine wanawaza. Matokeo inaweza kuwa nini kama mara kwa mara hatusikilize zamiri yetu na tunazoea kuvunja kanuni za Mungu? Kisha wakati fulani, zamiri yetu haitatusumbua tena kama tunafanya mambo ya mubaya, itakuwa sawa vile ngozi ya mwili yenye imeunguzwa kwa “chuma cha moto cha kutilia alama,” yenye haisikiake tena kitu. (1 Timoteo 4:2) Lakini, zamiri yenye imezoezwa na Neno ya Mungu, inaweza kutuongoza muzuri.

7. Tunapaswa kufanya nini kama tunapenda kukamata maamuzi ya muzuri?

7 Kwa hiyo, kama tunapenda kukamata maamuzi ya muzuri, tunapaswa kujua Biblia muzuri na tunapaswa kujua kutumikisha mambo yenye tumejifunza. Hatupaswe kukamata maamuzi haraka-haraka. Lakini tunapaswa kutafuta kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yetu na kufikiri sana namna tunaweza kuzitumia. Hata wakati inatuomba tukamate maamuzi bila kukawia, sawa vile Shadraki, Meshaki, na Abednego, tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri kama tunajua Biblia muzuri na kama zamiri yetu imezoezwa muzuri. Tuone namna tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri mu sehemu mbili za maisha yetu.

Nani Njo Wanapaswa Kuwa Marafiki Wetu?

8, 9. (a) Ni kanuni gani zinaonyesha kuwa ni jambo ya maana kuepuka marafiki wabaya? (b) Marafiki wabaya ni wale tu wenye kuwa na mwenendo mubaya? Fasiria.

8 Mutume Paulo aliandika hivi: “Musidanganywe. Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.” (1 Wakorinto 15:33) Yesu Kristo aliambia wanafunzi wake hivi: “Hamuko sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19) Ile maandiko inatufundisha kama tunapaswa kuepuka kufanya urafiki na watu sawa vile waasherati, wazinifu, wezi, na walevi. (1 Wakorinto 6:9, 10) Wakati tunaendelea kuelewa Biblia muzuri, tunatambua kama tunapaswa pia kuepuka kuangalia wale watu mu filme, mu vipindi vya televizyo, ku Enternete ao kusoma vitabu nyenye kuwazungumuzia. Tunapaswa pia kuepuka kuzungumuza kupitia Enternete na “wale wenye kuficha namna wako.”​—Zaburi 26:4.

9 Tunaweza kufanya urafiki na watu wenye wanaonekana kuwa wako na mwenendo muzuri, lakini hawamutumikie Yehova? Biblia inatuambia hivi: “Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Tunaelewa kama marafiki wabaya haiko tu wale wenye kuwa na mwenendo mubaya. Njo maana, ni jambo ya hekima tufanye urafiki wa sana na watu tu wenye kumupenda Yehova.

10. Nini njo itatusaidia kuamua muzuri ikiwa ni lazima tupitishe wakati fulani na watu wenye hawamutumikie Yehova ao hapana?

10 Hatuwezi kuepuka watu wote wenye hawamutumikie Yehova, na Biblia haituambie tufanye vile. (Yohana 17:15) Tunakutanaka na watu wenye hawamutumikie Yehova wakati tunaenda mu mahubiri, ku masomo, na ku kazi. Na Mukristo mwenye bibi ao bwana yake haiko Shahidi, anaweza kulazimika kukutana mara kwa mara na watu wenye hawamutumike Yehova. Kama tunatumia nguvu zetu za utambuzi, tutaelewa kama kuko tofauti kati ya kukutana kwa wakati fulani na watu wenye hawamutumikie Yehova na kuwa marafiki wao wa sana. (Yakobo 4:4) Ile itatusaidia kuamua ikiwa tutafanya mambo mbalimbali na wanafunzi wenzetu kisha saa za masomo, sawa vile michezo ao dansi ao ikiwa tutaenda ku karamu zenye zinafanywa kwa ajili ya wafanyakazi.

Kuchagua Kazi

11. Nini njo tunapaswa kufikiria kwanza wakati tuko nachagula kazi yenye tutafanya?

11 Kutumikisha kanuni za Biblia kunaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri kuhusu namna tutatimiza daraka yetu ya kutolea watu wa familia yetu mahitaji yao. (1 Timoteo 5:8) Kwanza, tunapaswa kufikiria ni kazi ya aina gani njo tutakuwa nafanya. Tunajua kama ni mubaya kufanya kazi yenye itatulazimisha kufanya mambo yenye Biblia inasema waziwazi kuwa ni ya mubaya, sawa vile kuabudu sanamu, kuiba, kutumia damu mubaya, na mambo ingine yenye Biblia inakataza. Pia hatupaswe kusema uongo ao kutenda kwa udanganyifu, hata kama mukubwa wetu wa kazi anatuomba tufanye vile.​—Matendo 15:29; Ufunuo 21:8.

12, 13. Ni mambo gani ingine ya maana yenye tunapaswa kufikiria wakati tuko nakamata maamuzi kuhusu kazi?

12 Halafu kama kazi yenye tutafanya haitatuomba tufanye mambo yenye Biblia inakataza waziwazi? Wakati tunaendelea kuelewa Biblia muzuri zaidi, tunatambua kama kuko mambo ingine yenye tunapaswa kufikiria mbele tukamate maamuzi. Kwa mufano, tunaweza kujiuliza: Ni muzuri kuitika kazi ya kuitika ku telefone, fasi kwenye watu wanachezaka michezo ya feza? Unapaswa pia kufikiria makuta yenye watakuwa nakulipa itakua natoka wapi na utakua natumikia wapi. Kwa mufano ni muzuri kwa Mukristo mwenye iko na kazi yake, kukubali kazi ya kupakala rangi ku kanisa fulani, ile haitakuwa kuunga mukono dini ya uongo?​—2 Wakorinto 6:14-16.

13 Sasa, tutafanya nini kama mukubwa wetu wa kazi anatuomba upakale rangi ku kanisa? Kama ni vile, unaweza kufikiria kama utakatala ao ikiwa utafanya nini. Tuseme nini kuhusu kazi zenye hazipingane na kanuni za Biblia? Kwa mufano kupelekea watu barua mu eneo, kutia ndani fasi kwenye watu wanafanyaka mambo ya mubaya? Mambo yenye Biblia inasema mu Matayo 5:45 inaweza kukusaidia ukamate uamuzi muzuri? Tunaweza pia kujiuliza ikiwa zamiri yetu haitatusumbua wakati tutaendelea kufanya ile kazi. (Waebrania 13:18) Kwa kweli, juu tukamate maamuzi ya muzuri kuhusu kazi, tunapaswa kuzoeza nguvu zetu za utambuzi na zamiri yetu.

“Umutambue Katika Njia Zako Zote”

14. Tunapaswa kufanya nini mbele ya kukamata maamuzi?

14 Halafu maamuzi yenye tunakamataka kuhusu mambo ingine, sawa vile kusoma masomo ya juu ao kukubali ao kukatala matunzo fulani? Mbele ya kukamata maamuzi yoyote, tunapaswa kufikiria kanuni za Biblia zenye zinazungumuzia ile mambo, na kisha kufiria namna tutatumikisha zile kanuni. Sulemani, Mufalme mwenye hekima wa Israeli ya zamani, alisema hivi: “Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote, na usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.”​—Mezali 3:5, 6.

15. Mufano wa Wakristo wa kwanza-kwanza unatufundisha nini kuhusu kukamata maamuzi?

15 Mara mingi, maamuzi yenye tunakamata inaweza kuletea wengine faida ao kuwaletea magumu, na ile ni jambo yenye tunapaswa kufikiria. Kwa mufano, haikukuwa tena lazima kwa Wakristo wa kwanza-kwanza kufuata sheria za mingi zenye Mungu alipatiaka Waisraeli kuhusu chakula. Wangeweza kula chakula mbalimbali zenye sheria ilikataza ao ilisema kuwa haziko safi. Lakini, mutume Paulo aliandika hivi kuhusu nyama yenye inawezekana ilikuwa imetolewa kwanza kwa miungu ya uongo: “Kama chakula kinamukwaza ndugu yangu, mimi sitakula nyama tena hata kidogo, ili nisimukwaze ndugu yangu.” (1 Wakorinto 8:11-13) Paulo alitia moyo Wakristo wa kwanza-kwanza, wafikirie zamiri za wengine juu wasiwakwaze. Maamuzi yetu haipaswe kutufanya kuwa “vikwazo.”​—1 Wakorinto 10:29, 32.

Uombe Mungu Akupatie Hekima

16. Sala inaweza kutusaidia namna gani wakati tunataka kukamata maamuzi?

16 Ni muzuri tusali mbele tukamate maamuzi. Mwanafunzi Yakobo anasema hivi: “Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu na bila kulaumu, na atapewa hiyo.” (Yakobo 1:5) Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atajibia sala zetu, na atatupatia hekima yenye tuko nayo lazima juu ya kukamata maamuzi ya muzuri. Wakati tunaambia Yehova mambo yenye iko na tuhangaisha na kumuomba atusaidie, roho takatifu inaweza kutusaidia kuelewa maandiko na kutusaidia kukumbuka maandiko yenye pengine tumesahau.

17. Wengine wanaweza kutusaidia namna gani wakati tunataka kukamata maamuzi?

17 Wengine wanaweza kutusaidia wakati tunataka kukamata maamuzi? Ndiyo, Yehova ametupatia ndugu na dada wenye hekima. (Waefeso 4:11, 12) Tunaweza kuwaomba mashauri zaidi sana wakati tunataka kukamata uamuzi wa maana sana. Wale ndugu na dada wenye wamejionea mambo mingi mu maisha na wenye wanaelewa Biblia muzuri, wanaweza kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri na ‘uhakikishe mambo ya maana zaidi.’ (Wafilipi 1:9, 10) Lakini, tukumbuke kama haiko wao njo wanapaswa kutukamatia maamuzi. Tunapaswa kubeba muzigo wetu wenyewe.

Maamuzi ya Muzuri Inaletaka Matokeo ya Muzuri Kila Mara?

18. Maamuzi ya muzuri inaletaka matokeo ya muzuri kila mara? Fasiria

18 Maamuzi yenye kutegemea Biblia inaletaka matokeo ya muzuri kila mara? Ndiyo, ku mwisho, inaletaka tu matokeo ya muzuri. Hata kama ku mwanzo inaweza kutuletea magumu. Shadraki, Meshaki, na Abednego walijua kama kukatala kuabudu ile sanamu kungefanya wauwawe. (Danieli 3:16-19) Vilevile, kisha mitume kuambia Sanhedrini ya Wayahudi kama ni lazima wamutii Mungu kuliko wanadamu, walipigwa fimbo mbele ya kuachiliwa. (Matendo 5:27-29, 40) Zaidi ya ile, tukumbuke kama “wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.” Ile inaweza kufanya maamuzi yetu isikuwe na matokeo yenye tuliwazia. (Muhubiri 9:11) Kama tunateseka kwa njia fulani, hata kama tulikamata maamuzi ya muzuri, tujue kama Yehova atatupatia nguvu ya kuvumilia na ku mwisho, atatubariki.​—2 Wakorinto 4:7.

19. Tunapaswa kufanya nini juu tuweze kubeba muzigo wetu kwa kukamata maamuzi yenye hekima?

19 Wakati tunakamata maamuzi, tunapaswa kuchunguza kanuni za Biblia na kufikiria namna tutatumikisha zile kanuni. Tunamushukuru sana Yehova juu iko tayari kutusaidia kupitia roho yake takatifu na kupitia ndugu na dada wenye hekima! Tuendelee basi kufuata muongozo wa Yehova, na kutumia musaada wenye ametupatia juu tuendelee kubeba muzigo wetu kwa kukamata maamuzi yenye hekima.

Umejifunza Nini?

• Tunapaswa kufanya nini juu tukamate maamuzi ya muzuri?

• Namna gani kukomala kiroho kunatusaidia tuchague marafiki wetu?

• Tunapaswa kufikiria mambo gani wakati tuko nakamata maamuzi kuhusu kazi?

• Ni mambo gani inaweza kutusaidia wakati tunataka kukamata maamuzi?

[Maulizo ya Funzo]

[Picha]

Makosa ya Adamu na Eva inatufundisha jambo fulani ya maana sana

[Picha]

Mbele ya kukamata maamuzi ya maana, chunguza kanuni za Biblia