Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kuhusu Ufalme wa Mungu

Kuhusu Ufalme wa Mungu

Tunayojifunza Kutoka Kwa Yesu

Kuhusu Ufalme wa Mungu

Ufalme wa Mungu ni nini?

Ufalme wa Mungu ni serikali ambayo itatawala dunia yote. Yesu alisema: “Basi, ninyi msali hivi: . . . ‘Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’”—Mathayo 6:9, 10; Danieli 2:44.

Ni nani watakaokuwa watawala wa Ufalme wa Mungu?

Yesu alizaliwa ili awe Mtawala wa Ufalme wa Mungu. Malaika alimwambia hivi mama ya Yesu: “Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.” (Luka 1:30-33) Kwa kuongezea, Yesu alichagua baadhi ya wafuasi wake ili watawale pamoja naye. Aliwaambia mitume wake: “Ninyi ndio mmeshikamana nami katika majaribu yangu; nami ninafanya agano pamoja nanyi, sawa na vile Baba yangu alivyofanya agano pamoja nami, kwa ajili ya ufalme.” (Luka 22:28, 29; Danieli 7:27) Jumla ya wafuasi 144,000 wa Yesu ndio watakaotawala pamoja naye.—Ufunuo 5:9, 10; 14:1.

Serikali hiyo itakuwa wapi?

Ufalme wa Mungu utatawala kutoka mbinguni. Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Nikienda na kuwatayarishia ninyi mahali [mbinguni], nitakuja tena nami nitawapokea ninyi nyumbani kwangu mwenyewe, ili mahali nilipo mimi, ninyi pia muwe hapo. . . . Ninaenda kwa Baba.”—Yohana 14:2, 3, 12; Danieli 7:13, 14.

Ufalme wa Mungu utachukua hatua gani ili kukomesha uovu?

Yesu atawaondoa watu wote waovu duniani. Yesu alisema hivi: “Wakati Mwana wa binadamu [Yesu] atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake . . . Na hawa [waovu] watakatiliwa mbali milele, lakini waadilifu wataingia katika uzima wa milele.”—Mathayo 25:31-34, 46.

Ni nani watakaoishi duniani wakiwa raia wa Ufalme huo?

Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairithi dunia.” (Mathayo 5:5; Zaburi 37:29; 72:8) Dunia itajaa watu ambao hata sasa wanajifunza kupendana. Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake: “Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda ninyi, ninyi nanyi mpendane vivyo hivyo. Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”—Yohana 13:34, 35.

Ufalme wa Mungu utawafanyia nini wanadamu duniani?

Yesu ataponya magonjwa yanayowakumba wanadamu. Yesu alipokuwa duniani, alizungumza na umati wa watu kuhusu “ufalme wa Mungu, naye akawaponya wale wanaohitaji kuponywa.” (Luka 9:11) Baada ya kumuona Yesu aliyefufuliwa katika maono, mtume Yohana alisema: “Nikaona mbingu mpya na dunia mpya . . . Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu . . . Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena.’”—Ufunuo 21:1-4.

Ufalme wa Mungu utaifanya dunia iwe Paradiso. Mtenda-maovu mmoja aliyeuawa pamoja na Yesu alisema: “Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” Naye Yesu akamwambia: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”—Luka 23:42, 43; Isaya 11:4-9.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? *

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 16 Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.