Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Mungu Ni Mtu Halisi?

Je, Mungu Ni Mtu Halisi?

Je, Mungu Ni Mtu Halisi?

Watu wengi wanajibu hivi:

▪ “Yuko kila mahali, katika kila kitu. Yeye ni kama upepo.”

▪ “Yeye ni nguvu fulani isiyoonekana yenye akili ambayo si mtu halisi.”

Yesu alisema nini?

▪ “Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi.” (Yohana 14:2) Yesu alisema Mungu ana nyumba, au mahali pa kuishi pa mfano.

▪ “Mimi nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni. na zaidi ya hayo, ninauacha ulimwengu nami ninaenda kwa Baba.” (Yohana 16:28) Yesu aliamini kwamba Mungu ni Mtu halisi anayeishi mahali fulani hususa.

YESU hakuwahi kusema kwamba Mungu ni nguvu fulani isiyoonekana. Badala ya hivyo, alizungumza na Mungu na kusali kwake. Mara nyingi alisema Yehova ni Baba yake wa mbinguni, maneno yaliyoonyesha uhusiano wake wa karibu sana pamoja na Mungu.—Yohana 8:19, 38, 54.

Ni kweli kwamba “hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote” na kwamba “Mungu ni Roho.” (Yohana 1:18; 4:24) Lakini hilo halimaanishi kwamba hana umbo au mwili wa aina fulani. Biblia inatuambia: “Ikiwa kuna mwili wa nyama, kuna wa roho pia.” (1 Wakorintho 15:44) Basi je, Yehova ana mwili wa roho?

Ndiyo. Yesu alipofufuliwa “aliingia mbinguni kwenyewe, ili sasa aonekane mbele za uso wa Mungu kwa ajili yetu.” (Waebrania 9:24) Hilo linatufundisha mambo mawili muhimu kumhusu Mungu. Kwanza, anaishi mahali fulani. Pili, yeye ni Mtu, si nguvu fulani isiyoonekana iliyo kila mahali.

Hivyo, basi, ni jinsi gani Mungu anaweza kuongoza mambo kila mahali? Mungu anaweza kutuma roho takatifu, au nguvu za utendaji, mahali popote ulimwenguni. Kama baba anayewanyooshea watoto wake mkono ili awatulize na kuwategemeza, Mungu anatumia roho yake takatifu ili kutimiza kusudi lake.—Zaburi 104:30; 139:7.

Kwa kuwa Mungu ni Mtu, yeye ana utu unaopendezwa na kuchukizwa na vitu fulani, na hata ana hisia. Biblia inatuambia kwamba anawapenda watu wake, anashangilia katika kazi zake, anachukia ibada ya sanamu, na kuumia kwa sababu ya uovu. (Mwanzo 6:6; Kumbukumbu la Torati 16:22; 1 Wafalme 10:9; Zaburi 104:31) Andiko la 1 Timotheo 1:11 linamwita “Mungu mwenye furaha.” Haishangazi kwamba Yesu alisema tunaweza kuja kumpenda Mungu kwa moyo wetu wote!—Marko 12:30. *

[Maelezo ya chini]

^ fu. 12 Kwa habari zaidi kuhusu jambo hilo, ona sura ya 1 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Blabu katika ukurasa wa 5]

Kama baba anayenyoosha mkono wake, Mungu anatumia roho yake takatifu ili kutimiza kusudi lake