Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kuzaliwa Upya—Je, Ni Muhimu?

Kuzaliwa Upya—Je, Ni Muhimu?

Kuzaliwa Upya—Je, Ni Muhimu?

KATIKA mazungumzo yake yote na Nikodemo, Yesu alikazia kwamba kuzaliwa upya, au kuzaliwa tena, ni muhimu sana. Alisema nini ili kuonyesha jambo hilo waziwazi?

Ona jinsi Yesu alivyokazia umuhimu wa kuzaliwa upya alipozungumza na Nikodemo. Alisema: “Mtu asipozaliwa tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3) Maneno “asipozaliwa tena” na “hawezi” yanaonyesha kwamba ni lazima mtu azaliwe upya. Kwa mfano: Mtu akisema, “Jua lisipowaka, hakuwezi kuwa na mwangaza wa mchana,” anamaanisha kwamba ni lazima jua liwake ili kuwe na mwangaza wa mchana. Vivyo hivyo, Yesu alisema kwamba kuzaliwa tena ni jambo la lazima kabisa ili kuuona Ufalme wa Mungu.

Kisha Yesu akasema, “Ninyi lazima mzaliwe tena,” kana kwamba anataka kuondoa shaka yoyote kuhusu kuzaliwa tena. (Yohana 3:7) Ni wazi kwamba kulingana na Yesu kuzaliwa tena ni takwa—jambo la lazima—ili mtu ‘aingie katika Ufalme wa Mungu.’—Yohana 3:5.

Kwa kuwa Yesu aliona kuzaliwa upya kuwa jambo muhimu sana, Wakristo wanapaswa kuhakikisha kwamba wanaelewa jambo hili kwa usahihi. Kwa mfano, je, unafikiri Mkristo anaweza kuchagua kuzaliwa tena?

[Blabu katika ukurasa wa 5]

“Jua lisipowaka, hakuwezi kuwa na mwangaza wa mchana”