Ona video zinazopatikana

Yesu Ni Mungu?

Yesu Ni Mungu?

Watu wengi wanawazaka kama fundisho ya utatu “njo musingi wa mafundisho yote ya Kikristo.” Ile fundisho inaonyesha kama, Baba, Mwana, na roho takatifu, ni watu watatu katika Mungu mumoja. Kardinale John O’Connor alisema hivi juu ya utatu: “Ile fundisho ni fumbo na hatuwezi kuielewa.” Juu ya nini fundisho ya utatu inakuwaka nguvu sana kuelewa?

KitabuThe Illustrated Bible Dictionary inatuambia sababu moja. Inasema hivi juu ya utatu: “Haiko fundisho ya Biblia juu hakuna andiko hata moja yenye inaizungumuzia.” Juu fundisho ya utatu “haipatikane mu Biblia,” wale wenye kufundisha ile fundisho wako nafanya yao yote juu ya kutafuta maandiko yenye inaunga mukono ile fundisho. Na hata wanafasiria mubaya maandiko juu tu ionekane kama inaunga mukono ile fundisho.

Kuko Andiko ya Biblia Yenye Inaunga Mukono Fundisho ya Utatu?

Kwa mufano, andiko yenye mara mingi inatumiwaka mubaya, ni Yohana 1:1. Ile andiko iko na aina mbili ya neno ya Kigiriki the·osʹ (mungu). Neno ya kwanza iko na kibainishi wazi ao article défini ton, na ile inaonyesha kama neno the·onʹ inamaanisha Mungu Mweza-yote. Lakini, neno ya pili, the·osʹ haina kibainishi wazi. Ile ni kosa?

Juu ya nini fundisho ya utatu inakuwaka nguvu sana kuelewa?

Injili ya Yohana iliandikwa mu Koine, Kigiriki ya watu wa kawaida. Koine iko na sheria zenye kuwa wazi juu ya namna ya kutumia kibainishi wazi. A. T. Robertson, mutu mwenye elimu ya Biblia, anaonyesha kama ikiwa sehemu ya musemwa yenye kuonyesha mutu ao kitu, na sehemu yenye inatoa maelezo juu ya ule mutu ao kile kitu ziko na vibainishi, “ni kusema zote mbili ziko wazi, zinalingana, ziko sawa sawa, na moja inaweza kukamata nafasi ya ingine.” Robertson anatumia Matayo 13:38 ili kufasiria ile jambo. Ile andiko inasema hivi: “Shamba [Kigiriki, ho a·grosʹ] ni ulimwengu [Kigiriki, ho koʹsmos].” Kulingana na sarufi ya luga ya Kigiriki, neno shamba na neno ulimwengu, ziko na maana moja.

Lakini, tuseme nini kama, sehemu ya musemwa yenye kuonyesha mutu ao kitu njo iko na kibainishi, lakini sehemu yenye kutoa maelezo juu ya ule mutu ao kile kitu haina kibainishi sawa vile inaonekana mu Yohana 1:1? Wakati anazungumuzia ile andiko, James Allen Hewett, mutu mwenye elimu ya Biblia, anasema hivi: “Mu ile musemwa, sehemu yenye inaonyesha mutu ao kitu, na sehemu yenye inatoa maelezo juu ya ule mutu ao kile kitu havilingane, haviko sawa sawa hata kidogo.”

Hewett anatumia 1 Yohana 1:5 ili kufasiria ile jambo. Ile andiko inasema hivi: “Mungu ni mwangaza.” Mu ile andiko, neno “Mungu” inatafsiriwa ho the·osʹ mu Kigiriki, ni kusema iko na kibainishi. Lakini neno phos yenye inatafsiriwa “mwangaza” haina kibainishi. Hewett anasema hivi: “Mutu . . . anaweza kusema Mungu ni mwangaza; lakini hawezi kusema mwangaza ni Mungu.” Mufano ingine yenye kuonyesha ile jambo inapatikana mu Yohana 4:24, yenye inasema “Mungu ni roho.” Na ingine inapatikana mu 1 Yohana 4:16, yenye inasema “Mungu ni upendo.” Mu ile maandiko mbili, sehemu ya musemwa yenye kuonyesha mutu iko na kibainishi wazi, lakini sehemu yenye kutoa maelezo juu ya mutu, ni kusema, “Roho” na “upendo,” haina kibainishi wazi. Ni kusema sehemu ya musemwa yenye kuonyesha mutu haiwezi kukamata nafasi ya sehemu yenye kutoa maelezo juu ya ule mutu; na sehemu yenye kutoa maelezo juu ya mutu haiwezi kukamata nafasi ya sehemu yenye kuonyesha mutu. Njo maana ile maandiko haiwezi kumaanisha “Roho ni Mungu” ao “upendo ni Mungu.”

“Neno” Ni Nani?

Watu wengi wenye elimu ya Kigiriki ya zamani na watafsiri wa Biblia wanasema kama Yohana 1:1 haionyeshe “Neno” ni nani. Lakini inaonyesha Neno ni mutu wa namna gani. William Barclay, mutafsiri wa Biblia, anasema hivi: “Juu [mutume Yohana] hatumie kibainishi wazi mbele ya neno theos, ni kusema ile neno inatoa tu maelezo . . . Yohana haseme kama Neno iko sawasawa na Mungu. Haseme kama Yesu alikuwa Mungu.” Jason David BeDuhn, mutu mwenye elimu, anasema pia hivi: “Mu Kigiriki, kama hautie kibainishi wazi mbele ya neno theos mu ile musemwa yenye kuwa mu Yohana 1:1c, wasomaji wako watawaza kama uko tu nazungumuzia ‘mungu fulani tu.’ . . . . Juu neno theos haina kibainishi wazi, iko tofauti na ho theos, sawa vile mu Kiswahili ‘mungu’ yenye inaanza na herufi ya kidogo iko tofauti na ‘Mungu’ yenye inaanza na herufi kubwa.” BeDuhn anaongezea hivi: “Mu Yohana 1:1, Neno haiko ule Mungu mumoja tu, lakini ni mungu, ao mwenye kuwa na hali ya kimungu.” Joseph Henry Thayer, mwenye alisaidiaka kutafsiri American Standard Version, anasema hivi juu ya ile jambo: “Logos [ao, Neno] alikuwa wa hali ya kimungu, hapana Mungu mwenyewe.”

Yesu alionyesha wazi kama haiko sawasawa na Baba yake

Kujua Mungu ni nani “inapaswa kuwa fumbo kabisa”? Yesu hakukuwa na ile mawazo. Wakati alisali kwa Baba yake, alionyesha watu waziwazi kama yeye haiko sawa na Baba yake. Alisema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3) Kama tunamuamini Yesu na tunaelewa mafundisho ya Biblia yenye kuwa wazi, tutamuheshimia na kumuona sawa vile Mwana wa Mungu. Na tena tutamuabudu Yehova, yeye njo “Mungu wa pekee wa kweli.”