Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu Ashinda Vishawishi

Yesu Ashinda Vishawishi

Kwa Ajili ya Vijana Wetu

Yesu Ashinda Vishawishi

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi.

CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA MATHAYO 4:1-11.

Fafanua jangwa alimokaa Yesu kwa siku 40.

․․․․․

Wazia sauti ya Mshawishi. Sauti yake inaonyesha ana mwelekeo gani? Namna gani sauti ya Yesu?

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Shetani alifanya jambo gani linaloonyesha kwamba anatumia nafasi yoyote anayopata kwa faida yake mwenyewe? (Soma tena mstari wa 2.)

․․․․․

Kwa nini Ibilisi hakumtolea Yesu falme zote tu, bali pia ‘utukufu wake’? (Soma tena mstari wa 8.)

․․․․․

Huenda Shetani alikuwa na kusudi gani alipomshawishi Yesu kwa kumtolea nafasi ya kuutawala ulimwengu?

․․․․․

(a) Kila kishawishi cha Shetani kinaonyesha nini kuhusu mawazo yake? ․․․․․

(b) Kwa upande mwingine, kila jibu la Yesu linaonyesha nini kuhusu mawazo yake? ․․․․․

TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Wakati hasa kishawishi kinapoweza kutokea.

․․․․․

Njia mbalimbali ambazo Shetani anaweza kutumia kutushawishi.

․․․․․

Jinsi tunavyoweza kushinda vishawishi.

․․․․․

NI JAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBALO LIMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․