Ona video zinazopatikana

Ujikaze Kukomala Kiroho Juu “Siku Kubwa ya Yehova Iko Karibu”

Ujikaze Kukomala Kiroho Juu “Siku Kubwa ya Yehova Iko Karibu”

Ujikaze Kukomala Kiroho Juu “Siku Kubwa ya Yehova Iko Karibu”

“Tusonge mbele kuelekea ukomavu.”​—EBR. 6:1.

1, 2. Juu ya nini Wakristo wa Yudea walipaswa kukimbia na nini njo iliwapatia nafasi ya kukimbia?

 WKATI Yesu alikuwa ku dunia, wanafunzi wake walimukaribia na kumuuliza hivi: “Na ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?” Wakati Yesu aliwajibia, alizungumuzia unabii wenye ungetimia kwa mara ya kwanza mu karne ya kwanza. Yesu alizungumuzia tukio fulani yenye haiko ya kawaida yenye ingeonyesha kama mwisho ilikuwa karibu kabisa. Wakati wangeona ile tukio, “wale wenye kuwa katika Yudea [walipaswa] kukimbilia kwenye milima.” (Mt. 24:1-3, 15-22) Wanafunzi wa Yesu wangetambua alama yenye aliwapatia na kufuata maagizo yake?

2 Miaka 30 hivi kisha pale, ni kusema mu mwaka 61 kisha kuzaliwa kwa Yesu, mutume Paulo aliandika ujumbe muzito kwa ajili ya Wakristo Waebrania wenye walikuwa naishi Yerusalemu na mu maeneo yenye ilikuwa karibu na Yerusalemu. Ile wakati Paulo na waamini wenzake hawakujua kama alama yenye ingeonyesha mwanzo wa “taabu kubwa” ingeanza kutimia kisha tu miaka tano hivi. (Mt. 24:21) Mu mwaka wa 66 kisha kuzaliwa kwa Yesu, majeshi ya Roma yenye iliongozwa na Sesho Galo, ilikuja kushambulia Yerusalemu. Lakini bila kutazamia, iliondoka na ile ikapatia Wakristo nafasi ya kukimbia.

3. Paulo alipatia Wakristo Waebrania shauri gani, na juu ya nini?

3 Wale Wakristo walipaswa kuwa na utambuzi na kuwa macho kiroho juu waweze kuelewa maana ya matukio na kukimbia. Lakini, Wakristo fulani walikuwa “wazito katika kusikia [kwao].” Walikuwa sawa vile watoto wadogo wenye wako na lazima ya “maziwa.” (Soma Waebrania 5:11-13.) Hata Wakristo fulani wenye walikuwa walishafanya miaka mingi katika kweli, walikuwa nafanya mambo yenye ilionyesha kama wako ‘najitosha kwa Mungu mwenye kuishi.’ (Ebr. 3:12) Wakristo fulani walikuwa na “desturi” ya kukosa mikutano mu ile kipindi yenye ile “day [was] drawing near.” (Ebr. 10:24, 25) Shauri yenye Paulo aliwapatia ilifika kwa wakati wenye kufaa kabisa. Aliwaambia hivi: “Kwa kuwa sasa tumeacha nyuma fundisho la musingi juu ya Kristo, tusonge mbele kuelekea ukomavu.”​—Ebr. 6:1.

4. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuwa macho kiroho, na nini njo itatusaidia kufanya vile?

4 Tunaishi wakati ya utimizo ya mwisho wa unabii wa Yesu. “Ile siku kubwa ya Yehova,” siku yenye ataharibu ulimwengu wa Shetani, “iko karibu.” (Sef. 1:14) Hii njo wakati kabisa ya kuwa macho kiroho. (1 Pe. 5:8) Tuko macho kiroho? Kukomaa kiroho njo kutatusaidia tuendelee kukumbuka kama tunaishi mu siku za mwisho.

Kukomala Kiroho Maana Yake Nini?

5, 6. (a) Kukomala kiroho maana yake nini? (b) Tunapaswa kufanya mambo gani mbili juu tukomale kiroho?

5 Paulo aliambia Wakristo wa wakati wa mitume wakomale kiroho na aliwaambia pia maana ya kukomala kiroho. (Soma Waebrania 5:14.) “Watu wakomavu” hawatoshekake tu na “maziwa,” lakini wanakulaka pia “chakula kigumu.” Kwa hiyo, wanajua “mambo ya musingi” na “mambo mazito” ya Maandiko. (1 Ko. 2:10) Zaidi ya ile, nguvu zao za utambuzi zinazoezwa wakati wanatumia mambo yenye wanajua juu ya kutofautisha mema na mabaya. Wakati wanataka kukamata maamuzi, wanatafuta kwanza kujua kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yao na kisha wanatumikisha zile kanuni.

6 Mutume Paulo aliandika hivi: “Ni lazima tukaze uangalifu zaidi kuliko kawaida juu ya mambo yenye tulisikia, ili tusipeperushwe mbali hata kidogo.” (Ebr. 2:1) Tunaweza kupeperushwa mbali bila hata kujua. Juu ile jambo isitufikie, tunapaswa kukaza “more than the usual attention” wakati tuko najifunza Biblia. Kwa hiyo, kila mutu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Ningali tu najifunza mambo ya musingi? Ninapendaka kabisa kusoma Biblia, ao ninasomaka-somaka tu bila kufikiria mambo yenye niko nasoma? Nini njo itanisaidia nifanye maendeleo ya kiroho kwa moyo wote?’ Juu tukomale kiroho, kuko mambo mbili yenye tunapaswa kufanya: Tunapaswa kujua muzuri Neno ya Mungu, na tunapaswa kujifunza kutii.

Ujue Muzuri Neno ya Mungu

7. Tutapata faida gani kama tunajua muzuri Neno ya Mungu?

7 Mutume Paulo aliandika hivi: “Kila mutu mwenye anaendelea kunywa maziwa hajue neno la haki, kwa maana yeye ni mutoto mudogo.” (Ebr. 5:13) Juu tukomale kiroho, tunapaswa kujua muzuri Neno ya Mungu. Juu Biblia njo iko na mawazo ya Mungu, tunapaswa kujifunza Biblia kwa bidii na pia vichapo vya “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45-47) Kujifunza Biblia vile, kutatusaidia tuzoeze nguvu zetu za utambuzi. Fikiria mufano wa Mukristo mwenye kuitwa Orchid. * Anasema hivi: “Wakati nilianza kusoma Biblia kila siku, ilinisaidia kubadilisha maisha yangu. Nilisoma Biblia yote kwa miaka mbili, lakini ilikuwa sawa vile njo ninaanza kujua muzuri Muumbaji wangu. Nilijifunza juu ya njia zake, mambo yenye anapendaka na yenye anachukiaka, uwezo mingi sana wenye iko nao, na hekima yake yenye haina mipaka. Kusoma Biblia kila siku kumenisaidia kupambana na hali za nguvu sana zenye nimekutana nazo mu maisha.”

8. Kusoma Neno ya Mungu kunaweza kutusaidia namna gani?

8 Kusoma kwa ukawaida sehemu fulani ya Neno ya Mungu, kutafanya mawazo yake ikuwe na ‘nguvu’ mu maisha yetu. (Soma Waebrania 4:12.) Ile inaweza kutusaidiea tubadilishe namna yetu ya kuwa na tumufurahishe Yehova zaidi. Unajiachiaka wakati ya kutosha ya kusoma Biblia na kufikiri sana juu ya mambo yenye inasema?

9, 10. Kujua Maandiko njo nini? Leta mufano.

9 Kujua muzuri Biblia haiko tu kujua mambo yenye inasema. Wakristo wenye Paulo aliita watoto kiroho, walikuwa najua mambo yenye Maandiko inasema. Lakini, hawakutumikisha ile mambo. Hawakuruhusu iwaongoze juu iwasaidie kukamata maamuzi ya hekima mu maisha yao.

10 Kujua Maandiko ni kujua mambo yenye Biblia inasema na kuitumikisha mu maisha yetu. Mambo yenye ilifikia dada Mukristo mwenye kuitwa Kyle inaonyesha namna tunaweza kufanya vile. Kyle alikosana na mufanyakazi mwenzake. Alifanya nini juu arudishe amani? Anasema hivi: “Palepale nilikumbuka andiko ya Waroma 12:18, yenye inasema: ‘Kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani na watu wote.’ Kwa hiyo, nilipanga kuzungumuza na mufanyakazi mwenzangu kisha saa za kazi.” Mazungumuzo ilipita muzuri, na ule mufanyakazi alifurahi kuona hatua yenye Kyle alikamata. Kyle anasema hivi: “Nilijifunza kama ikiwa tunatumikisha kanuni za Biblia, mambo itaendeka tu muzuri.”

Ujifunze Kutii

11. Nini njo inaonyesha kama inaweza kuwa nguvu kutii wakati tuko mu hali ya nguvu?

11 Haiko mwepesi kutumikisha mambo yenye Maandiko inasema, zaidi sana kama tuko mu hali ya nguvu. Kwa mufano, wakati kidogo tu kisha Yehova kutosha Waisraeli mu utumwa wa Misri, “wakaanza kugombana na Musa” na wakaendelea “kumujaribu Yehova.” Juu ya nini walifanya vile? Juu walikosa maji ya kunywa. (Kut. 17:1-4) Kulikuwa hakuyapita hata miezi mbili, tangu wafanye agano pamoya na Mungu na kukubali kama watatii “maneno yote yenye Yehova amesema.” Lakini, walikosa kumutii Mungu na walianza kuabudu sanamu. (Kut. 24:3, 12-18; 32:1, 2, 7-9) Juu ya nini walivunja ahadi yao? Pengine walifanya vile juu waliogopa kwa sababu Musa alikuwa amekawia ku Mulima Horebu? Ao pengine waliogopa kama Waamaleki watawashambulia na Musa hatakuwa pale juu ya kuwasaidia, sawa vile alikuwa amewasaidia? (Kut. 17:8-16) Hata sababu ikuwe nini, Waisraeli “walikataa kumutii” Mungu. (Mdo. 7:39-41) Paulo aliambia Wakristo ‘wafanye nguvu yao yote’ juu ‘wasianguke katika mufano uleule wa kukosa kutii,’ wenye Waisraeli waliangukia ndani wakati waliogopa kuingia mu inchi ya ahadi.​—Ebr. 4:3, 11.

12. Namna gani Yesu alijifunza kutii, na ile ilikuwa na matokeo gani?

12 Juu tukomale kiroho, tunapaswa kufanya yetu yote juu tumutii Yehova. Mufano wa Yesu unaonyesha kama, mara mingi tunajifunzaka kutii wakati tuko mu magumu. (Soma Waebrania 5:8, 9.) Mbele Yesu akuye ku dunia, alikuwa natii baba yake. Lakini, wakati alikuwa ku dunia, haikukuwa mwepesi kutii juu iliomba avumilie maumivu ya mingi na mahangaiko ya mingi. Juu Yesu alitii mu zile hali za nguvu sana, ‘alifanywa kuwa mukamilifu,’ ni kusema, alionyesha kuwa anastahili cheo yenye Mungu alikuwa napenda kumupatia, cheo ya kuwa Mufalme na Kuhani Mukubwa.

13. Nini njo itaonyesha kama tumejifunza kutii?

13 Halafu siye? Tunapenda kabisa kumutii Yehova, hata wakati tuko na magumu yenye iko natuhangaisha? (Soma 1 Petro 1:6, 7.) Mungu ametupatia mashauri yenye kuwa wazi, juu ya kuwa wanyoofu, kutumia muzuri ulimi wetu, kusoma na kujifunza Biblia kipekee, kuhuzuria mikutano, na kuhubiri. (Yos. 1:8; Mt. 28:19, 20; Efe. 4:25, 28, 29; 5:3-5; Ebr. 10:24, 25) Tuko namutii Yehova mu ile mambo yote, hata wakati tuko na magumu? Wakati tunatii tunaonyesha kama tunakomala kiroho.

Kukomala Kiroho Kuko na Faida Gani?

14. Namna gani kukomala kiroho kunaweza kutulinda? Leta mufano.

14 Kama tunazoeza nguvu zetu za utambuzi juu ya kutofautisha mema na mabaya, ile inaweza kutulinda juu tusiambukizwe na tabia za mubaya za watu wa ulimwengu huu, wenye “kuishiwa na ufahamu wote wa mambo yenye kuwa sawa.” (Efe. 4:19) Kwa mufano, ndugu mwenye kuitwa James, mwenye alikuwa nasoma vichapo vyetu kwa ukawaida na kufikiri juu ya mambo yenye alikuwa nasoma, alikubali kazi yenye wafanyakazi wengine wote, walikuwa wanamuke. James anasema hivi: “Hata kama wanamuke wengi walikuwa na mwenendo mubaya, mwanamuke fulani alikuwa na mwenendo muzuri na alionyesha kama anapendezwa na mambo yenye Biblia inafundisha. Lakini wakati tulikuwa tu miye naye mu chumba fulani ya kufanyia kazi, alianza kunitongoza. Niliwaza iko nafanya muzaha, lakini haikukuwa mwepesi kumuzuia. Palepale nikakumbuka mufano fulani yenye ilizungumuziwaka mu Munara wa Mulinzi juu ya ndugu mwenye alipataka ileile jaribu ku kazi. Ileile habari ilizungumuziaka mufano wa Yosefu na bibi wa Potifa. Palepale nikasukuma ule mwanamuke, na akakimbia.” (Mwa. 39:7-12) James alifurahi sana juu hawakufika mbali na juu aliendelea kuwa na zamiri ya muzuri.​—1 Ti. 1:5.

15. Namna gani kukomala kiroho kunaweza kutusaidia tushikamane sana na Yehova?

15 Kukomala kiroho kunaweza pia kutusaidia tushikamane na Yehova na ‘tusipotoshwe na mafundisho mbalimbali na yenye kuwa mageni.’ (Soma Waebrania 13:9.) Wakati tunajikaza kufanya maendeleo ya kiroho, akili yetu inakazia “mambo ya maana zaidi.” (Flp. 1:9, 10) Ile inafanya tufurahie zaidi mambo yote yenye Mungu iko natufanyia. (Ro. 3:24) Mukristo mwenye ‘mutu muzima katika uelewaji wake,” anakuwaka mwenye shukrani na anakuwaka na urafiki wa sana na Yehova.​—1 Ko. 14:20.

16. Nini njo ilisaidia dada fulani akomalishe ‘moyo wenye kuwa imara’?

16 Dada mwenye kuitwa Louise anasema kama, kwa wakati fulani kisha kubatizwa, alikuwa namutumikia Yehova juu tu ya kufurahisha wengine. Anasema hivi: “Sikukuwa nafanya mambo ya mubaya, lakini sikukuwa tu na hamu sana ya kumutumikia Yehova. Nilitambua kama nilipaswa kufanya mabadiliko fulani juu nimutumikie Yehova kwa moyo wangu wote. Badiliko kubwa yenye nilipaswa kufanya, ni kutia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yangu.” Juu dada Louise alijikaza kufanya vile, alikomalisha ‘moyo wenye kuwa imara,’ na ile ilimusaidia wakati alipambana na tatizo fulani ya afya yenye ilimuhangaisha sana. (Yak. 5:8) Dada Louise alisema hivi: “Haikukuwa mwepesi kabisa, lakini nilimukaribia Yehova zaidi.”

‘Mukuwe Watiifu Kutoka Katika Moyo’

17. Juu ya nini Wakristo wa Yerusalemu walipaswa kutii?

17 Shauri ya Paulo kuhusu ‘kusonga mbele kuelekea ukomavu’ iliokoa Wakristo wa kwanza-kwanza wenye walikuwa naishi Yerusalemu na Yudea. Wale wenye walisikiliza ile shauri, walikuwa macho kiroho. Ile iliwasaidia watambue alama yenye Yesu aliwapatia, yenye ilionyesha kama walipaswa “kukimbilia kwenye milima.” Wakati waliona “lile chukizo lenye linaleta uharibifu limesimama mahali patakatifu,” ni kusema, wakati waliona majeshi ya Roma inazunguka muji wa Yerusalemu, walijua kama walipaswa kukimbia. (Mt. 24:15, 16) Mwanahistoria wa mambo ya dini mwenye kuitwa Eusebius alionyesha kama Wakristo wenye walisikiliza onyo ya Yesu, walitoka Yerusalemu mbele iharibiwe na wakakimbilia mu muji wa Pela, wenye ulikuwa mu eneo ya milima ya Gileadi. Kwa kufanya vile, waliokoka musiba wenye ulipata muji wa Yerusalemu. Ule ulikuwa musiba mukubwa zaidi wenye ulifikiaka ule muji.

18, 19. Juu ya nini utii ni wa lazima leo?

18 Kukomala kiroho kutatusaidia tukuwe watiifu, na ile itaokoa uzima wetu wakati unabii wa Yesu wenye kuonyesha kama “kutakuwa taabu kubwa” utatimia mu dunia yote. (Mt. 24:21) Tutakuwa tayari kutii bila kukawia maagizo yenye tutapokea kutoka kwa “musimamizi-nyumba muaminifu”? (Lu. 12:42) Kwa kweli, hii njo wakati ya kujifunza ‘kuwa watiifu kutoka katika moyo’!​—Ro. 6:17.

19 Juu tukomale kiroho, tunapaswa kuzoeza nguvu zetu za utambuzi. Tunafanya vile kwa kujikaza kujua muzuri maandiko na kujifunza kutii.

[Maelezo ya chini]

^ Majina fulani imebadilishwa.

Ulijifunza Nini?

• Kukomala kiroho maana yake nini, na tunaweza kufanya nini juu tufikie kukomala kiroho?

• Juu ya nini ni jambo ya maana tujue muzuri Maandiko juu tukomale kiroho?

• Nini njo inaonyesha kama tumejifunza kutii?

• Kukomala kiroho kuko na faida gani?

[Maulizo ya Funzo]

[Picha]

Kutumikisha mashauri ya Biblia kunaweza tusaidia tumalize matatizo ya kukosa kuelewana kwa njia yenye kufaa

[Picha]

Kufuata mashauri ya Yesu kulisaidia Wakristo wa kwanza-kwanza waokoke