Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mtu Aliyekuwa na Imani Katika Ahadi za Mungu

Mtu Aliyekuwa na Imani Katika Ahadi za Mungu

Kwa Ajili ya Vijana Wetu

Mtu Aliyekuwa na Imani Katika Ahadi za Mungu

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi.

CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA MWANZO 12:1-4; 18:1-15; 21:1-5; 22:15-18.

Eleza jinsi ambavyo huenda Abrahamu alihisi aliposikia ahadi ya Mungu ya kwamba angekuwa babu ya “uzao” ambao ungeunufaisha ulimwengu wote.

․․․․․

Unafikiri wale wageni watatu wanaotajwa katika Mwanzo 18:2 walionekana jinsi gani?

․․․․․

Unafikiri utendaji unaotajwa katika Mwanzo 18:6-8 ulitukia namna gani? (Kumbuka kwamba Abrahamu alikuwa na umri wa miaka karibu 100 wakati huo.)

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Ni miaka mingapi ilipita kuanzia wakati ambapo Yehova alimwahidi Abrahamu mwana mpaka wakati ambapo Isaka alizaliwa? (Soma tena Mwanzo 12:4 na 21:5.)

․․․․․

Katika kipindi hicho chote cha kungoja Yehova alimhakikishia Abrahamu nini? (Soma Mwanzo 12:7; 13:14-17; 15:1-5, 12-21; 17:1, 2, 7, 8, 15, 16.)

․․․․․

Yehova alifanya nini Abrahamu alipoonyesha kwamba alikuwa na shaka kuhusu kumpata mwana? (Soma tena Mwanzo 15:3-5, 12-21.)

․․․․․

Yehova alifunua jinsi gani habari kuhusu ule “uzao” hatua kwa hatua?

․․․․․

TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Uhitaji wa kuwa na imani katika ahadi za Mungu.

․․․․․

Jinsi Yehova anavyofunua mapenzi yake hatua kwa hatua.

․․․․․

NI JAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBALO NI LA MAANA ZAIDI KWAKO, NA KWA NINI?

․․․․․