Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Epuka Kukengeushwa Fikira Katika Hii “Siku ya Habari Njema”

Epuka Kukengeushwa Fikira Katika Hii “Siku ya Habari Njema”

Epuka Kukengeushwa Fikira Katika Hii “Siku ya Habari Njema”

WALE watu wanne wenye ukoma walifikiria jambo la kufanya. Hakuna mtu yeyote aliyewapa msaada katika lango la jiji. Wasiria waliozingira jiji walizuia vyakula visiingizwe Samaria ili watu wasalimu amri au wafe njaa. Hakukuwa na sababu ya kuingia katika jiji hilo; chakula kiliuzwa kwa bei ya juu sana. Hata ilisemekana kwamba mwanamke fulani alimla mwana wake.—2 Fal. 6:24-29.

Wenye ukoma hao wakafikiria, ‘Kwa nini tusiende kwenye kambi ya Wasiria? Hatutapata hasara yoyote.’ Waliondoka wakati wa giza la jioni ili waingie katika kambi hiyo. Walipofika katika kambi hiyo, hakukuwa na kelele yoyote. Walinzi hawakuwapo. Farasi na punda walikuwa wamefungwa, lakini hakukuwa na askari-jeshi. Watu hao wanne wenye ukoma wakaangalia ndani ya hema moja. Hakukuwa na mtu yeyote ndani yake, lakini kulikuwa na chakula kingi na vinywaji. Wakala na kunywa. Wenye ukoma hao pia waliona dhahabu, fedha, mavazi, na vitu vingine vyenye thamani. Walivichukua, wakavificha, na kurudi kuchukua vitu zaidi. Kambi yote ilikuwa imeachwa bila mtu. Kwa njia ya kimuujiza, Yehova alikuwa amefanya Wasiria wasikie sauti ya jeshi la kivita. Wasiria walifikiri kwamba wanashambuliwa, hivyo wakakimbia. Waliacha vitu vyao vyote bila ulinzi!

Wenye ukoma hao walikuwa wanachukua vitu vyenye thamani na kuvificha. Hata hivyo, dhamiri yao ilianza kuwasumbua walipokumbuka kwamba watu walikuwa wanakufa njaa katika jiji jirani la Samaria. Wakaanza kuambiana hivi: “Jambo tunalofanya si sawa. Leo ni siku ya habari njema!” Wenye ukoma hao walirudi haraka Samaria na kuripoti habari njema kuhusu vitu walivyopata.—2 Fal. 7:1-11.

Sisi pia tunaishi katika ile inayoweza kuitwa “siku ya habari njema.” Kuhusu sehemu ya pekee ya ile “ishara . . . ya umalizio wa mfumo wa mambo,” Yesu alisema hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mt. 24:3, 14) Hilo linapaswa kutuchochea kwa njia gani?

Mahangaiko ya Kibinafsi Yanaweza Kutulemea

Wale watu wenye ukoma walishangilia sana walipopata vitu vyenye thamani hivi kwamba walisahau Samaria kwa muda. Walikazia fikira vitu ambavyo wangeweza kupata. Je, inaweza kuwa hivyo kwetu? “Upungufu wa chakula” ni sehemu ya ishara yenye matukio mengi ya kipindi cha umalizio wa mfumo wa mambo. (Luka 21:7, 11) Yesu aliwaonya wanafunzi wake hivi: “Jiangalieni ninyi wenyewe kwamba mioyo yenu isilemewe kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana na mahangaiko ya maisha.” (Luka 21:34) Tukiwa Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiruhusu mahangaiko ya kibinafsi kuhusu maisha ya kila siku yatufanye tusahau uhakika wa kwamba tunaishi katika “siku ya habari njema.”

Mkristo anayeitwa Blessing hakuruhusu mahangaiko yake yamlemee. Alitumika akiwa painia, akamaliza masomo yake, mwishowe akaolewa na Mwanabetheli, kisha akakubaliwa kuwa mshiriki wa familia ya Betheli ya Benin. Anasema hivi: “Ninatunza vyumba, na ninafurahia sana mgawo wangu.” Sasa Blessing anafurahi anapofikiria miaka 12 ambayo amekuwa katika utumishi wa wakati wote, naye anathamini kwamba amekazia fikira “siku ya habari njema” ambayo sasa hivi tunaishi ndani yake.

Jihadhari na Mambo ya Kukengeusha Fikira Yanayochukua Wakati

Yesu alisema hivi alipowatuma wale wanafunzi 70: “Kwa kweli, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Luka 10:2) Kama vile tu kuchelewa wakati wa mavuno kunavyoweza kusababisha hasara, vivyo hivyo kupuuza kazi ya kuhubiri kunaweza kufanya watu wapoteze uhai wao. Hivyo, Yesu aliongezea hivi: “Msimkumbatie mtu yeyote mkimsalimu barabarani.” (Luka 10:4) Neno la lugha ya awali ambalo limetafsiriwa kuwa ‘salimu’ linamaanisha mengi zaidi ya kusema tu “hujambo” au “uwe na siku njema.” Linaweza pia kutia ndani kumkumbatia rafiki mara nyingi na kuzungumza kwa muda mrefu unapokutana naye. Hivyo, Yesu aliwaagiza wafuasi wake waepuke kukengeushwa fikira isivyo lazima na kutumia vizuri wakati wao. Ujumbe ambao walipaswa kuhubiri ulikuwa wa haraka.

Fikiria muda tunaoweza kupoteza kwa sababu ya mambo yenye kukengeusha fikira. Kwa miaka mingi, televisheni imekuwa kifaa kinachopoteza wakati mwingi kuliko vifaa vingine vyote. Lakini namna gani simu za mkononi na kompyuta? Uchunguzi uliohusisha watu wazima 1,000 nchini Uingereza ulionyesha kwamba “Mwingereza wa kawaida anatumia dakika 88 kwa siku akiongea kwa simu ya kawaida, dakika nyingine 62 akiongea kwa simu ya mkononi, dakika 53 akituma barua-pepe na dakika 22 akituma ujumbe kwa simu ya mkononi.” Muda huo ukijumlishwa unazidi kwa mara mbili muda ambao painia msaidizi anatumia kila siku katika huduma! Unatumia muda mwingi kadiri gani kuwasiliana kwa njia hizo?

Ernst na Hildegard Seliger walikuwa waangalifu kuhusu walivyotumia wakati wao. Wote wawili walikaa katika kambi ya mateso ya Wanazi na magereza ya Wakomunisti kwa miaka zaidi ya 40. Baada ya kuachiliwa huru, walitumika wakiwa mapainia mpaka walipokufa wakiwa na tumaini la kwenda mbinguni.

Watu wengi walitaka kuwasiliana na Ndugu na Dada Seliger. Wenzi hao wa ndoa wangetumia saa nyingi kwa siku wakisoma na kuandika barua. Hata hivyo, walitanguliza mambo ya kiroho katika maisha yao.

Bila shaka, sote tunathamini sana kudumisha mawasiliano pamoja na wapendwa wetu, na hakuna kosa lolote kufanya hivyo. Kuna faida ya kufanya mambo mbalimbali yanayofaa kila siku. Hata hivyo, ni jambo la hekima kuwa macho ili kupunguza mambo yenye kukengeusha fikira yanayopoteza wakati mwingi katika siku hii ya kuhubiri habari njema.

Hubiri Habari Njema kwa Ukamili

Ni baraka kama nini kuishi katika “siku ya habari njema.” Acheni tusikengeushwe fikira kama wale wenye ukoma wanne walivyokengeushwa fikira mwanzoni. Kumbuka kwamba walikata kauli hivi: “Jambo tunalofanya si sawa.” Vivyo hivyo, si sawa kwetu kuruhusu miradi ya kibinafsi au mambo yenye kukengeusha fikira yanayopoteza wakati mwingi yatuzuie tusishiriki kikamili katika huduma.

Tuna mfano bora kabisa wa kufuata kuhusiana na hilo. Akikumbuka miaka 20 ya kwanza ya huduma yake, mtume Paulo aliandika hivi: “Nimehubiri kikamili habari njema juu ya Kristo.” (Rom. 15:19) Paulo hakuruhusu chochote kipunguze bidii yake. Acheni tuwe na bidii kama Paulo tunapotangaza ujumbe wa Ufalme katika hii “siku ya habari njema.”

[Picha katika ukurasa wa 28]

Blessing hakuruhusu mahangaiko yake yaingilie utumishi wake wa wakati wote

[Picha katika ukurasa wa 29]

Ndugu na Dada Seliger walikuwa waangalifu kuhusu walivyotumia wakati wao