Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Je, kuna tumaini lolote kwamba mtoto anayefia ndani ya tumbo la uzazi atafufuliwa?

Uhai unaanza wakati mimba inapotungwa. Yehova anaweza kumfufua mtu hata ikiwa uhai wake ulikuwa katika hatua gani ya maisha kwa sababu “mambo yote yanawezekana kwa Mungu.” (Marko 10:27) Lakini Biblia haisemi waziwazi ikiwa Yehova atawafufua watoto ambao walikufa wakiwa ndani ya tumbo la uzazi.—4/15, ukurasa wa 12, 13.

• Ni jambo gani lenye faida tunalojifunza kutokana na chungu, wibari, nzige, na mjusi?

Viumbe hao wanne wana hekima ya kisilika. Kwa hiyo, wanaonyesha kwamba Mungu ana hekima. (Met. 30:24-28)—4/15, ukurasa wa 16-19.

• Ni jambo gani la maana sana ambalo lilifanywa na Mashahidi wa Yehova miaka 100 iliyopita?

Mwaka wa 1909, shirika la kisheria la Mashahidi wa Yehova (Watch Tower Bible and Tract Society) lilihamishwa kutoka Pittsburgh, Pennsylvania, hadi Brooklyn, New York, ambako bado liko.—5/1, ukurasa wa 22-24.

• kwa nini Biblia inasema vizuri kuhusu kukaa kimya?

Inaonyesha kwamba kukaa kimya kunaweza kuwa ishara ya heshima, uthibitisho wa busara na utambuzi, na pia ni njia inayotusaidia kutafakari. (Zab. 37:7; 63:6; Met. 11:12)—5/15, ukurasa wa 3-5.

• John Wycliffe, William Tyndale, Robert Morrison, na Adoniram Judson walifanya nini?

Wote walilipenda Neno la Mungu na walilitafsiri katika lugha ambazo watu wa kawaida wangeweza kusoma. Wycliffe na Tyndale walilitafsiri katika Kiingereza, Morrison katika Kichina, na Judson katika Kiburma (Myanmar).—6/1, ukurasa wa 8-11.

• Ni wafalme wangapi wa Yuda ambao walikuwa na bidii sana kwa ajili ya nyumba ya Mungu?

Ufalme wa kusini wa Yuda ulitawaliwa na wafalme 19, na wanne kati yao ndio waliokuwa na bidii sana kwa ajili ya nyumba ya Mungu, yaani, Asa, Yehoshafati, Hezekia, na Yosia.—6/15, ukurasa wa 7-11.

• Je, Wakristo wote waliotiwa mafuta ambao wako duniani leo wanashiriki katika kutayarisha chakula cha kiroho?

Hapana. Wote ambao wametiwa mafuta kwa roho ya Mungu ni sehemu ya jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara, lakini wale wanaofanyiza Baraza Linaloongoza ndio wanaosimamia kazi ya kutayarisha chakula cha kiroho.—6/15, ukurasa wa 22-24.

• kwa nini vazi la ndani la Yesu liliwavutia sana askari-jeshi Waroma?

Askari-jeshi waliokuwapo wakati wa kifo cha Yesu hawakulirarua vazi lake vipande-vipande. Kwa kawaida, koti refu lisilo na mikono kama hilo lilishonwa kwa kuunganisha vitambaa viwili, lakini vazi la Yesu lilikuwa limefumwa kwa kitambaa kimoja, na hivyo lilikuwa na thamani kubwa zaidi.—7/1, ukurasa wa 22.

• kwa nini tunaweza kusema kwamba upendo ndiyo sifa kuu zaidi iliyomtofautisha Yesu na viongozi wa kidini?

Badala ya kuwapenda watu wa kawaida, viongozi hao waliwadharau. Zaidi ya hilo, hawakumpenda Mungu. Yesu alimpenda Baba yake na aliwasikitikia watu. (Mt. 9:36) Alikuwa mchangamfu, mwenye huruma, na aliwatendea watu kwa fadhili.—7/15, ukurasa wa 15.

• Huenda wenzi wa ndoa wakakabili matatizo gani kuhusu kupanga matumizi ya pesa, na ni nini kinachoweza kuwasaidia wafanikiwe?

Mara nyingi ugomvi kuhusu pesa unasababishwa na kutoaminiana au woga, na pia huenda wenzi wa ndoa wakawa na malezi tofauti. Mambo manne yanayoweza kuwasaidia kufanikiwa ni: Kujifunza kuzungumza kwa utulivu kuhusu pesa, kukubaliana juu ya maoni ambayo wanapaswa kuwa nayo kuhusu mshahara, kuandika mipango ya matumizi ya pesa za familia, na kukubaliana kuhusu madaraka ya kila mmoja wao.—8/1, ukurasa wa 10-12.