Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hadithi ya Tano ya Uwongo: Maria Ni Mama ya Mungu

Hadithi ya Tano ya Uwongo: Maria Ni Mama ya Mungu

Hadithi ya Tano ya Uwongo: Maria Ni Mama ya Mungu

Ni nini chanzo cha hadithi hiyo? “Kumwabudu mama ya Mungu kulianza wakati . . . wapagani wengi walipomiminika ndani ya kanisa. . . . Kwa maelfu ya miaka tayari wapagani hao [ambao waligeuka na kuwa Wakristo] walifahamu mambo ya dini na ya miungu kupitia ibada ya mungu wa kike, ‘mama mkuu’ na ‘bikira mtakatifu.’”—The New Encyclopædia Britannica (1988), Buku la 16, ukurasa wa 326 na 327.

Biblia inasema nini? “Utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu. . . . Kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.”—Italiki ni zetu; Luka 1:31-35, Union Version.

Andiko hilo linaonyesha wazi kwamba Maria alikuwa mama ya “Mwana wa Mungu,” wala si mama ya Mungu. Je, inawezekana kwamba Maria alikuwa amebeba ndani yake Yule ambaye ‘mbingu haziwezi kumtosha’? (1 Wafalme 8:27) Maria hakudai kamwe hivyo. Fundisho la Utatu ndilo hasa limeleta mvurugo kuhusu utambulisho wa Maria. Kwa kumtangaza kuwa Theotokos (neno la Kigiriki linalomaanisha “Aliyemzaa Mungu”), au “Mama ya Mungu,” Mkutano wa Efeso, uliofanywa mwaka wa 431 W.K., uliweka msingi wa kumwabudu Maria. Kwa karne nyingi, jiji la Efeso ambamo mkutano huo wa baraza la kanisa ulifanyiwa lilikuwa kitovu cha ibada ya sanamu ambako watu walisherehekea Artemi, mungu wa kike wa uzazi.

Kwa hiyo, mambo mengi ya ibada ya sanamu ya Artemi “iliyoanguka kutoka mbinguni,” kama vile misafara ya sherehe, yaliingizwa katika ibada ya Maria. (Matendo 19:35) Zoea lingine ambalo liliingizwa katika mafundisho ya Kikristo ni kutumia sanamu ya Maria na sanamu nyingine katika ibada.

Linganisha mistari hii ya Biblia: Mathayo 13:53-56; Marko 3:31-35; Luka 11:27, 28

UKWELI:

Maria alikuwa mama ya Mwana wa Mungu, bali si mama ya Mungu. Hadithi ya uwongo ya Utatu ilianzisha ibada ya Maria akiwa Mama ya Mungu